عن صُهيب بن سِنان الرومي رضي الله عنه مرفوعاً: «عجَبًا لِأَمر المُؤمِن إِنَّ أمرَه كُلَّه له خير، وليس ذلك لِأَحَد إِلَّا لِلمُؤمِن: إِنْ أَصَابَته سَرَّاء شكر فكان خيرا له، وإِنْ أَصَابته ضّرَّاء صَبَر فَكَان خيرا له».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Suhaibu bin Sinani Al Ruumiy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Ajabu iliyoje ya jambo la muumini, hakika jambo lake lote ni kheri, na hakuna hilo kwa yeyote ila kwa muumini: akipatwa na jambo lenye kufurahisha anashukuru ikawa hilo ni kheri kwake, na akipatwa na madhara anasubiri likawa hilo ni kheri kwake".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Alidhihirisha Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- mshangao kwa njia ya kuonyesha uzuri wa jambo la muumini; kwasababu yeye katika hali yake ya mabadiliko yake ya kidunia hatoki katika kheri na kusalimika na kufaulu, na kheri hii haiko kwa yeyote ila kwa muumini. Kisha akaeleza -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa muumini katika kila hali aliyoikadiri Mwenyezi Mungu juu yake ni kheri, akipatwa na madhara anasubiri kwakuwa ndio makadiro ya Mwenyezi Mungu, na anasubiri faraja toka kwa Mwenyezi Mungu, na anataraji malipo toka kwa Mwenyezi Mungu; likawa hilo ni kheri kwake. Na akipatwa na jambo la furaha miongoni mwa neema za dini; kama elimu na matendo mema, na neema za kidunia; kama mali na watoto na familia anamshukuru Mwenyezi Mungu, na hilo ni kwa kusimamia kumtii Mwenyezi Mungu -Aliyetakasika na kutukuka, anamshukuru Mwenyezi Mungu ikawa ni kheri kwake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno الدرية
Kuonyesha Tarjama