عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعًا: «يقول الله تعالى : ما لِعَبدِي المُؤمن عِندِي جَزَاء إِذَا قَبَضتُ صَفِيَّه مِنْ أَهلِ الدُّنيَا ثُمَّ احْتَسَبَه إِلاَّ الجنَّة».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hana mja wangu muumini toka kwangu malipo yoyote pindi ninapomchukua kipenzi chake katika familia yake duniani kisha akasubiri (malipo mazuri) zaidi ya pepo".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Anaeleza Nabii -Ziwe juu yake Amani- katika hadithil Qudsiy hii, kuwa yeyote atakayetahiniwa kwa kumkosa kipenzi chake miongoni mwa ndugu wa karibu au yeyote, atakaposubiri mwanadamu juu ya kuondokewa na yule aliyemteua na kumchagua na akaona kua huyu ndiye mwenye mahusiano mazuri na yeye, kama mtoto, au baba mdogo, au baba, au mama, au rafiki, anapomchukua Mwenyezi Mungu Mtukufu kisha mwanadamu akataraji malipo basi hana malipo mengine zaidi ya pepo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama