عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «قال الله عز وجل : أنا عند ظنِّ عَبدي بي، وأنا معه حيث يَذكُرني، والله، لَلَّه أَفرَحُ بِتَوبَةِ عَبدِهِ مِنْ أَحَدِكُم يَجدُ ضَالَّتَهُ بالفَلاَة، وَمَنْ تَقَرَّب إِلَيَّ شِبْرًا، تقرَّبتُ إليه ذِرَاعًا، ومن تقرب إلي ذِراعًا، تقربت إليه بَاعًا، وإذا أَقْبَلَ إِلَيَّ يمشي أَقْبَلْتُ إِلَيهِ أُهَرْوِلُ». متفق عليه، وهذا لفظ إحدى روايات مسلم. وروي في الصحيحين: «وأنا معه حِينَ يَذْكُرُنِي» بالنون، وفي هذه الرواية. «حيث» بالثاء وكلاهما صحيح.
[صحيح] - [متفق عليه وها لفظ مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Amesema Mwenyezi Mungu -Mtukufu- mimi niko katika dhana ya mja wangu kwangu, na mimi niko pamoja naye pindi anaponikumbuka, Namuapa Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu huwa na furaha zaidi kwa toba ya mja wake kuliko mmoja wenu anapompata mnyama wake aliyepotea katika ardhi ya jangwa kubwa, na atakayejiweka karibu yangu kiasi cha shibri moja (nusu futi) basi mimi nitakuwa karibu yake dhiraa nzima (futi nzima), Na atakayejiweka karibu yangu dhiraa moja basi nitakuwa karibu naye mita nzima, na akinijia kwa kutembea nitamjia nikiwa nakimbia". Hadithi Muttafaqun a'laihi, Na tamko hili ni moja ya riwaya za Muslim. Na imepokelewa katika sahihi mbili (Bukhariy na Muslim) "Na mimi niko pamoja naye pale anaponitaja" na zote ziko sahihi.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu yuko katika dhana ya mja wake kwake; akimdhania kheri basi atazipata, na ikiwa atamdhania ubaya basi ataupata, katika kitabu cha Musnadi cha Imamu Ahmadi katika hadithi za Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anasema: Amesema Mwenyezi Mungu -Mtukufu- (Mimi niko katika dhana ya mja wangu kwangu, ikiwa atanidhania kheri basi ataipata, na ikiwa atanidhania shari basi ataipata) Lakini ni wakati gani atamdhania Mwenyezi Mungu kheri? Atamdhania Mwenyezi Mungu vizuri pale atakapofanya yale yanayopelekea kupata fadhila za Mwenyezi Mungu na matumaini yake, akafanya mema na akamdhania vizuri Mwenyezi Mungu kuwa atayapokea, ama akimdhania vizuri kisha akakaa asifanye lolote; Hii ni katika kutamani toka kwa Mwenyezi Mungu, na atakayeifuata nafsi yake matamanio yake na akajipa matumaini kwa Mwenyezi Mungu basi huyo ni mtu asiyejitambua, Na ama kumdhania vizuri Mwenyezi Mungu pamoja nakuwa unapambana naye kwa kumuasi, hii ni njia ya watu wasiofikiria ambao hawana mtaji wanaojipa matarajio kupitia huo. Amesema bin Qayyim -Mwenyezi Mungu Amrehemu-: "Hakuna shaka kuwa na dhana nzuri ni lazima kuwe na kufanya vizuri, kwasababu mwenye kutenda wema anamdhania vizuri Mola wake kuwa atamlipa kwa wema wake, na haendi kinyume na ahadi yake, na anakubali toba yake. Ama mwenye kufanya mabaya mwenye kuendelea na madhambi makubwa na dhulma na kwenda kinyume na sheria mbali mbali, basi lile giza la maasi na dhulma na mambo ya haramu linamzuia kumdhania vizuri Mola wake, kwani mja aliyeangamia aliyetoka katika utiifu wa bwana yake hawezi kumdhania vizuri, na hawezi kukusanya mambo mawili giza la maovu na kuwa na dhana nzuri milele, kwani muovu huwa na hofu kwa kadiri ya uovu wake, Na katika watu wenye dhana nzuri zaidi kwa Mola wao ni wale wenye kumtii zaidi. kama alivyosema Hasan Al baswariy: Hakika muumini kamdhania Mola wake vizuri akafanya mazuri, na hakika mtu muovu kamdhania vibaya Mola wake akafanya mabaya" kisha akaeleza kuwa Mwenyezi Mungu huwa na furaha zaidi, yaani furaha inayoendana na utukufu wake Mtukufu kwa toba ya mja wake kuliko yule aliyepata alichopoteza, na kilichopotea ni kitu kilichokosekana, na hiyo pia ni jangwani, , na maana ya toba, ni kukiri na kujuta na kujivua na kuazimia mtu kuwa hatorudia yale aliyoyafanya. Kisha akataja kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ni mkarimu mno kuliko mja wake, anapojiweka karibu mwanadamu kwake kwa kiasi cha nusu futi; basi Mwenyezi Mungu anajiweka karibu naye futi nzima, na akijiweka karibu naye kwa futi moja yeye anakuwa karibu naye kwa mita nzima, na akimjia akiwa anatembea anamjia Mwenyezi Mungu Mtukufu akiwa ana kimbia, Hivyo yeye ana ukarimu mwingi na ni mwepesi wa kujibu kuliko mja wake. Na hadithi hii: Ni katika yale wanayoyaamini Ahlus sunnati waljama'a (wenye kufuata na mafundisho ya Mtume na maswahaba zake) kuwa haya ni kweli na hakika ni ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, lakini sisi hatujui kunakuwaje huku kukimbia, na kunakuwaje huku kuwa karibu, basi ni jambo ambalo namna yake inarudi kwa Mwenyezi Mungu, na hatuna nafasi ya kuzungumza ndani yake, lakini tunaamini maana yake na tunaikabidhi namna yake kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na kuwa pamoja kwa Mwenyezi Mungu na mja wake kuna aina mbili: Maalumu; kunako pelekea kupata ushindi na msaada , nayo ni hii iliyotajwa katika hadithi, na kwa ujumla kunako maanisha elimu ya kujua kwake na kukizingira kila kitu, nako ni kwa uhakika kunakoendana na Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri
Kuonyesha Tarjama
Ziada