عن عمر بن الخطاب رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم أنه قال: «لو أنكم كنتم توَكَّلُون على الله حق توَكُّلِهِ لرزقكم كما يرزق الطير، تَغْدُو خِمَاصَاً، وتَرُوحُ بِطَاناَ».
[صحيح] - [رواه الترمذي وابن ماجه وأحمد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Omari bin Khattwabi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake; kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- yakwamba yeye Amesema: "Laiti nyinyi mgetegemea kwa Mwenyezi Mungu ukweli wa kumtegemea, basi angekuruzukuni kama anavyowaruzuku ndege, wanatoka asubuhi wakiwa na njaa, wanarudi jioni wakiwa wameshiba"
Sahihi - Imepokelewa na Ibnu Maajah
Inatuelekeza hadithi hii kuwa tutegemee kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu katika mambo yetu yote, Na ukweli wa kutegemea ni: kuegemea kwa Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, katika kuleta manufaa na kuzuia madhara katika mambo ya kidunia na ya Akhera; kwasababu hakuna awezae kutoa wala kuzuia wala kudhuru wala kunufaisha ispokuwa yeye aliyetakasika na kutukuka, nakuwa mwanadamu yeye kafanya sababu za kuleta manufaa na kumzuilia madhara pamoja na kumtegemea Mwenyezi Mungu: "Na mwenye kumtegemea Mwenyezi Mungu basi yeye humtosha", "Na kwake basi na wategemee wenye kutegemea" wakati wowote mja akilifanya hilo basi Mwenyezi Mungu atamruzuku kama anavyowaruzuku ndege ambao wanatoka asubuhi nao wakiwa na njaa na wanarudi jioni nao wakiwa wamejaza matumbo yao.