عن عمر بن الخطاب رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم أنه قال: «لو أنكم كنتم توَكَّلُون على الله حق توَكُّلِهِ لرزقكم كما يرزق الطير، تَغْدُو خِمَاصَاً، وتَرُوحُ بِطَاناَ».
[صحيح] - [رواه الترمذي وابن ماجه وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Omari bin Khattwabi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake; kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- yakwamba yeye Amesema: "Laiti nyinyi mgetegemea kwa Mwenyezi Mungu ukweli wa kumtegemea, basi angekuruzukuni kama anavyowaruzuku ndege, wanatoka asubuhi wakiwa na njaa, wanarudi jioni wakiwa wameshiba"
Sahihi - Imepokelewa na Ibnu Maajah

Ufafanuzi

Inatuelekeza hadithi hii kuwa tutegemee kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu katika mambo yetu yote, Na ukweli wa kutegemea ni: kuegemea kwa Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, katika kuleta manufaa na kuzuia madhara katika mambo ya kidunia na ya Akhera; kwasababu hakuna awezae kutoa wala kuzuia wala kudhuru wala kunufaisha ispokuwa yeye aliyetakasika na kutukuka, nakuwa mwanadamu yeye kafanya sababu za kuleta manufaa na kumzuilia madhara pamoja na kumtegemea Mwenyezi Mungu: "Na mwenye kumtegemea Mwenyezi Mungu basi yeye humtosha", "Na kwake basi na wategemee wenye kutegemea" wakati wowote mja akilifanya hilo basi Mwenyezi Mungu atamruzuku kama anavyowaruzuku ndege ambao wanatoka asubuhi nao wakiwa na njaa na wanarudi jioni nao wakiwa wamejaza matumbo yao.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa kutegemea, nakuwa hiyo ni katika sababu kubwa zinazotumiwa kuvuta riziki.
  2. Kutegemea hakupingani na kufanya sababu, kwasababu yeye ameeleza kuwa kutegemea kwa kweli hakuendi kinyume na kutoka asubuhi na kurudi jioni katika kutafuta riziki.
  3. Kutilia umuhimu sheria matendo ya moyoni; kwasababu kutegema ni amali ya moyoni.
  4. Kutegemea kwa Mwenyezi Mungu ni sababu ya kimaana (isiyoonekana) katika kuleta riziki na wala haipingani na kufanya sababu za kihisia (zinazoonekana).
  5. Sheria ya kutegemea kwa Mwenyezi Mungu katika mahitaji yote, nayo ni katika mambo ya wajibu katika imani, Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na kwa Mwenyezi Mungu basi tegemeeni ikiwa nyinyi ni waumini -kweli-".