عن أبي مسعود البدري رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «مَنْ قَرَأَ بِالآيَتَيْنِ مِنْ آخر سُورَةِ البَقَرَةِ في لَيْلَةٍ كَفَتَاه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Na kutoka kwa Abii Masudi Al-Badriy- radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kutoka kwa Mtume rehema na Amani zimfikie, amesema: "Atakayezisoma aya mbili za mwisho wa suratul Baqara katika wakati wa usiku zitamtosheleza".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Ameeleza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa atakayesoma aya mbili za mwisho wa suratul Baqara katika wakati wa usiku kabla ya kulala kwake basi hakika Mwenyezi Mungu atamtosheleza na shari na yale yenye kuchukiza, na inasemekana katika maana ya kumtosheleza: Yaani kuhusu kusimama usiku, au zitamtosheleza na nyiradi zingine, au alikusudia kuwa zenyewe ni kiasi kidogo ambacho kinaweza kumtosheleza na kusoma aya zingine katika kisimamo cha usiku, na yasemekana kinyume na hivyo, na yote yaliyotajwa ni sahihi yanakusanywa na tamko.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kubainishwa ubora wa mwisho wa suratul-Baqara.
  2. Mwisho wa suratul-Baqara kunazuia kwa msomaji wake mabaya na shari na shetani atakaposoma nyakati za usiku.