عن ابن عباس رضي الله عنهما مرفوعاً: «عَيْنَانِ لاَ تَمسُّهُمَا النَّار: عَيْنٌ بَكَتْ من خَشْيَة الله، وعَيْنٌ بَاتَت تَحْرُسُ في سَبِيل الله».
[صحيح] - [رواه الترمذي]
المزيــد ...

Kutoka kwa bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Hadithi Marfu'u: "Macho ya aina mbili hautoyagusa moto: Jicho lililolia kwa kumuogopa Mwenyezi Mungu, na jicho lililokesha likilinda kwaajili ya Mwenyezi Mungu".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Maana ya hadithi: Nikuwa moto hautogusa jicho lililolia kwa kumuogopa Mwenyezi Mungu Mtukufu, hivyo pindi anapokumbuka mtu ukubwa wa Mwenyezi Mungu na uwezo wake juu ya waja wake na uzembe wake katika haki za Mwenyezi Mungu Mtukufu; akalia kwa kutaraji rehema zake na kuogopa adhabu zake na hasira zake, basi huyu kaahidiwa kusalimika na moto. Na jicho jingine ambalo moto hautoligusa, nalo ni: Yule atakayelala akilinda kwaajili ya Mwenyezi Mungu katika mipaka au sehemu ya mapigano kwa kuhifadhi roho za waislamu. Na kauli yake: "Hautoyagusa moto" Hii ni katika sehemu ya kutaja sehemu ya kitu na makusudio yake ni chote: nakuwa atakayelia kwa kumuogopa Mwenyezi Mungu Mtukufu na atakayelala akilinda katika njia ya Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu Mtukufu anaiharamisha miili yao katika moto.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama