عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «سبق المُفَرِّدُونَ» قالوا: وما المُفَرِّدُونَ ؟ يا رسول الله قال: « الذاكرون الله كثيرا والذاكراتِ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- "Wametangulia watu wa kipekee" Wakasema: Ni akina nani watu wa kipekee? Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Wenye kumtaja Mwenyezi Mungu kwa wingi wanaume na wenye kumtaja wanawake".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Maana ya hadithi: Nikuwa wenye kumtaja Mwenyezi Mungu kwa wingi wanaume na wanawake, wametofautiana na wengine, wameshinda kwa kupata ujira kwasababu ya kukithiri kushughulika kwao na kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu, wao wamefanya zaidi ya wengine; wakawa ndio waliotangulia zaidi katika kheri. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na wenye kumtaja Mwenyezi Mungu wanaume, na wenye kumtaja wanawake, amewaandalia Mwenyezi Mungu msamaha na ujira mkubwa). Hivyo kauli yake: "Wenye kumtaja Mwenyezi Mungu kwa wingi wanaume" Yaani: Nyakati nyingi, hasa hasa nyakati za nyiradi maalumu, kama asubuhi na mchana, na mwisho wa swala za faradhi.