عن أبي هريرة رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: « رَغِمَ أنْفُ، ثم رَغِمَ أنْفُ، ثم رَغِمَ أنْفُ من أدرك أبويه عند الكِبر، أحدهما أو كِليهما فلم يدخل الجنة».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: "Ameangukia pua (kapata hasara), kisha Ameangukia pua (kapata hasara), kisha Ameangukia pua (kapata hasara), atakayewapata wazazi wake wawili wakati wa ukubwa mmoja wao au wote wawili na akawa hakuingia peponi".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Haki ya wazazi wawili ni kubwa, ameiambatanisha Mwenyezi Mungu Mtukufu na haki yake ambayo kwaajili yake kawaumba viumbe hawa wenye akili: (Na muabuduni Mwenyezi Mungu na wala msimshirikishe na chochote na kwa wazazi wawili muwatendee wema) Akaamrisha Mwenyezi Mungu kuabudiwa na akawausia watoto na akawahimiza kuwafanyia wema wazazi wawili na kuwafanyia wema kwa kauli na matendo; na hiyo ni kwasababu ya kumsimamia kwao yeye na kuwalea kwao na kukesha kwaajili ya raha yao, na hakuna malipo mazuri ya wema zaidi ya wema. Na maana ya hadithi hii nikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- aliomba mara tatu juu ya yule atakayewadiriki wazazi wawili au mmoja wao na akawa hakuingia peponi kwasababu ya kutowafanyia wema, na kutowafanyia wema ni katika sababu za wazi kuingia motoni, na kuwaasi ni sababu ya kuingia motoni ikiwa kama hazitomfikia rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu-.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri الدرية
Kuonyesha Tarjama