عن أبي هريرة رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: « رَغِمَ أنْفُ، ثم رَغِمَ أنْفُ، ثم رَغِمَ أنْفُ من أدرك أبويه عند الكِبر، أحدهما أو كِليهما فلم يدخل الجنة».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Ameangukia pua (kapata hasara), kisha Ameangukia pua (kapata hasara), kisha Ameangukia pua (kapata hasara), atakayewakuta wazazi wake wawili wakati wa utuuzima, mmoja wao au wote wawili, na akawa hakuingia peponi".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Mtume rehema na amani ziwe juu yake aliomba dua ya udhalili na fedheha mpaka akahisi kana kwamba mtu ametia pua yake kwenye mchanga – akarudia mara tatu – akaulizwa: Ni nani huyo ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, uliyemuombea dua mbaya?
Akasema rehema na amani ziwe juu yake: Atakayewakuta wazazi wake wawili, mmoja wao au wote wawili, wakati wa utuuzima, wakawa si sababu ya yeye kuingia Peponi; na hii ni kutokana na kukosa kuwatendea wema na kutowatii.