عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «أقْرَبُ ما يَكون العبد مِنْ رَبِّهِ وهو ساجد، فَأَكْثروا الدُّعاء».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume- Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Mahala alipo karibu zaidi mja na Mola wake ni pale anapokuwa kasujudu, zidisheni dua".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume- Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Mahala alipo karibu zaidi mja na Mola wake ni pale anapokuwa kasujudu", Na hiyo ni kwasababu mtu anaposujudu, yeye huweka kiungo kitukufu mno katika viungo vyake mahala pa kuweka miguu ambapo hukanyagwa na miguu, na vile vile pia anaweka kiungo kilicho juu usawa wa kiungo kilichochini. Yaani: nikuwa uso wake ndio ulioko juu zaidi kuliko vingine katika viungo vyake, na visigino vyake ndivyo vilivyochini zaidi katika viungo vyake-, akaviweka katika usawa mmoja kwa unyenyekevu na kwa kujidhalilisha kwaajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwasababu hii ikawa ni mahala pa karibu zaidi na Mola wake anapokuwa kasujudu, ukakusanyika katika hilo mkao na maneno kwa kujinyenyekeza kwaajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwasababu hiyo anasema mwanadamu katika sijida yake: Ametakasika Mola wangu aliyejuu, Hii ni ishara kuwa yeye aliyetakasika na kutukuka ni Mtukufu aliyetukuka katika dhati yake na sifa zake, nakuwa mwanadamu ndiye aliyechini na mwenye kujishusha ukilinganisha na Utakasifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu na Utukufu wake.