عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «أقْرَبُ ما يَكون العبد مِنْ رَبِّهِ وهو ساجد، فَأَكْثروا الدُّعاء».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume- Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Mahala alipo karibu zaidi mja na Mola wake ni pale anapokuwa kasujudu, zidisheni dua".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume- Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Mahala alipo karibu zaidi mja na Mola wake ni pale anapokuwa kasujudu", Na hiyo ni kwasababu mtu anaposujudu, yeye huweka kiungo kitukufu mno katika viungo vyake mahala pa kuweka miguu ambapo hukanyagwa na miguu, na vile vile pia anaweka kiungo kilicho juu usawa wa kiungo kilichochini. Yaani: nikuwa uso wake ndio ulioko juu zaidi kuliko vingine katika viungo vyake, na visigino vyake ndivyo vilivyochini zaidi katika viungo vyake-, akaviweka katika usawa mmoja kwa unyenyekevu na kwa kujidhalilisha kwaajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwasababu hii ikawa ni mahala pa karibu zaidi na Mola wake anapokuwa kasujudu, ukakusanyika katika hilo mkao na maneno kwa kujinyenyekeza kwaajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwasababu hiyo anasema mwanadamu katika sijida yake: Ametakasika Mola wangu aliyejuu, Hii ni ishara kuwa yeye aliyetakasika na kutukuka ni Mtukufu aliyetukuka katika dhati yake na sifa zake, nakuwa mwanadamu ndiye aliyechini na mwenye kujishusha ukilinganisha na Utakasifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu na Utukufu wake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ni sunna kukithirisha dua katika sijida, kwasababu ni katika mahala pa kujibiwa dua.
  2. Utiifu unamzidishia mja ukaribu na Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na Kutukuka.
  3. Kila anapozidisha mja utiifu anapokea Mwenyezi Mungu dua zake.
  4. Pupa ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- juu ya kuufundisha umma wake kheri na sababu zake na milango yake.