عن أبي هريرة رضي الله عنه عن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: "كَلِمَتَانِ خفيفتان على اللسان، ثقيلتان في الميزان، حبيبتان إلى الرحمن: سبحان الله وبحمده، سبحان الله العظيم".
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Maneno mawili yanapendeka sana kwa Ar-Rahmani (Mwingi wa Rehema) ni mepesi sana katika ulimi, ni mazito sana katika mizani: Sub-haana llaahi wabihamdihi- Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema zake-, Sub-haana llaahil A'dhwiim- Ametakasika Mwenyezi Mungu Mtukufu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Ameeleza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithi hii kuwa Mola wetu Ar-Rahmani- Mwingi wa Rehema Aliyetakasika na kutukuka kuwa anayapenda maneno haya mawili yenye herufi chache pamoja na uzito wake katika mizani: Sub-haana llaahi wabihamdihi- Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema zake-, Sub-haana llaahil A'dhwiim- Ametakasika Mwenyezi Mungu Mtukufu; kwa yale yaliyokusanya ndani yake miongoni mwa tasbihi (kumtukuza Mwenyezi Mungu Mtukufu) na kumtakasa kutokana na mapungufu na yale yote yasiyoendana na Utukufu wake Aliyetakasika na kutukuka-, na msisitizo juu ya kumtakasa huku ni kumsifu kwa ukubwa na utukufu.