عن أبي هريرة رضي الله عنه عن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: "كَلِمَتَانِ خفيفتان على اللسان، ثقيلتان في الميزان، حبيبتان إلى الرحمن: سبحان الله وبحمده، سبحان الله العظيم".
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Maneno mawili yanapendeka sana kwa Ar-Rahmani (Mwingi wa Rehema) ni mepesi sana katika ulimi, ni mazito sana katika mizani: Sub-haana llaahi wabihamdihi- Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema zake-, Sub-haana llaahil A'dhwiim- Ametakasika Mwenyezi Mungu Mtukufu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Ameeleza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithi hii kuwa Mola wetu Ar-Rahmani- Mwingi wa Rehema Aliyetakasika na kutukuka kuwa anayapenda maneno haya mawili yenye herufi chache pamoja na uzito wake katika mizani: Sub-haana llaahi wabihamdihi- Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema zake-, Sub-haana llaahil A'dhwiim- Ametakasika Mwenyezi Mungu Mtukufu; kwa yale yaliyokusanya ndani yake miongoni mwa tasbihi (kumtukuza Mwenyezi Mungu Mtukufu) na kumtakasa kutokana na mapungufu na yale yote yasiyoendana na Utukufu wake Aliyetakasika na kutukuka-, na msisitizo juu ya kumtakasa huku ni kumsifu kwa ukubwa na utukufu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kufaa kutumia vina (katika uzungumzaji) kwa sharti la kutojilazimisha.
  2. Ubora wa maneno haya mawili katika kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  3. Kuthibitisha sifa ya kupenda kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu- kwa namna inayofaa kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  4. Kuthibitisha jina la Ar-Rahmani (Mwingi wa Rehema) kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  5. Kuhimizwa juu ya dhikiri hii yenye maneno machache na mema mengi.
  6. Nikuwa dhikiri zinatofautiana ubora, na sambamba na hilo ni kutofautiana malipo pia.
  7. Kuthibitisha mizani nakuwa ni kweli.
  8. Inapendeza kwa atakayemhamasisha mwenzie katika jambo la kheri basi amtajie sehemu ya faida zake.