Orodha ya Hadithi

Wallahi – akipenda Mwenyezi Mungu - sitokula kiapo cha jambo fulani isipokuwa ninapoona kilichobora zaidi basi huwa ninatoa kafara ya kiapo changu kisha ninafanya lililo bora zaidi.”
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
La kwanza litakalohukumiwa kati ya watu siku ya kiyama ni katika damu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Mwenye kupigana ili neno la Mwenyezi Mungu liwe juu, basi huyo yuko katika Njia ya Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Msivae hariri wala dibaji (Sufi) wala msinywe katika vyombo vya dhahabu au vya fedha, wala msile katika vyombo vilivyotengenezwa kwa dhahabu na fedha, kwani ni vyao (Makafiri) katika dunia na sisi ni vyetu Akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayevaa hariri duniani hatoivaa Akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakaye apa juu ya kiapo cha mila isiyokuwa ya uislamu kwa uongo tena kwa makusudi basi atakuwa kama alivyosema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ama mimi sikukuapisheni kwa sababu ya kuwatuhumu, lakini Jibril alinijia na kuniambia kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu anajifaharisha kupitia nyinyi, huko kwa Malaika.!
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika hao wawili wanaadhibiwa, na hawaadhibiwi kwa makosa makubwa, ama mmoja wao alikuwa hajistiri na mkojo, na ama mwingine alikuwa akitembea kwa kuchonganisha watu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mtakaposikia wito (Adhana), basi semeni mfano wa yale ayasemayo muadhini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ziache, kwani hakika mimi nimezivaa zikiwa safi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akipendezwa sana na kuanzia kulia, katika kuvaa kwake viatu, na kutana kwake nywele, na twahara yake, na katika mambo yake yote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Je anaweza kulala mmoja wetu akiwa na janaba? Akasema: Ndiyo, atakapotawadha mmoja wenu basi na alale
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
hakika hilonitatizolinatokananamshipawakizazikukatika, lakini acha swala kwa kiasi cha siku ulizokuwa ukipata hedhi ndani yake, kisha oga na swali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nyoosheni safu zenu, kwani hakika kunyoosha safu ni katika ukamilifu wa swala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakapotawadha mmoja wenu basi na aweke maji puani mwake kisha ayapenge, na atakayestanji kwa mawe basi afanye yawe witiri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Anapoingia mtu nyumbani kwake akamtaja Mwenyezi Mungu wakati wa kuingia kwake na wakati wa chakula chake, Shetani husema: Hakuna malazi kwenu, wala chakula cha usiku
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mchungeni(mfuatilieni) Muhammadi -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa watu wa nyumba yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika katika Jihadi kubwa ni kusema neno la uadilifu kwa kiongozi dhalimu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika dunia ni tamu, ni ya kijani, na hakika Mwenyezi Mungu anakumilikisheni ndani yake aone ni namna gani mtafanya, iogopeni dunia na waogopeni wanawake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
"Haya (Aibu) haiji ila kwa kheri"
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Sikumuona Mtume -rehema amani ziwe juu yake- katu akipitiliza kucheka mpaka kionekane Kilimi ndani ya mdomo wake, bali alikuwa akitabasamu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilihifadhi kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- rakaa kumi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake anapoamka usiku anasafisha kinywa chake kwa mswaki
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Paliletwa mashtaka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuhusu mtu anayepata wasiwasi kuwa anapata kitu ndani ya swala (katika vitenguzi vya udhu), Akasema: asiondoke mpaka asikie sauti, au apate harufu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Itakaposimamishwa swala na kikatengwa chakula cha usiku basi anzeni na chakula cha usiku
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hachukii muumini wa kiume tabia za muumini wa kike, akichukia tabia fulani basi ataridhishwa na tabia nyingine
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Mnapoingia chooni, msielekee Kibla, wala msikipe mgongo, bali elekeeni Mashariki au Magharibi.”
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Asishike mmoja wenu utupu wake kwa mkono wake wa kulia akiwa anakidhi haja ndogo, na asijifute haja ndogo au kubwa kwa mkono wake wa kulia na asipumulie ndani ya chombo anachonywea
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Amekataza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuswali baada ya swala ya sub-hi mpaka lichomoze jua, na baada ya laasiri mpaka lizame
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hivi haogopi mmoja wenu (Au: Hachelei mmoja wenu) atakapoinua kichwa chake kabla ya imamu, Mwenyezi Mungu akifanye kichwa chake kuwa kichwa cha punda, au aifanye Mwenyezi Mungu sura yake kuwa sura ya punda
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakuwa mtu mmoja alimuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu Kiyama, akasema: Lini Kiyama? Akasema: “Umetayarisha nini kwa ajili yake?”
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Alikuwa akinyanyua mikono yake usawa wa mabega yake anapofungua swala,
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alinifundisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake, namna ya tashahudi iletwayo ndani ya sala, na kiganja changu kikiwa kati ya viganja vyake, kama anavyonifundisha sura ndani ya Qur'ani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Allaahumma inniy a'udhubika min adhaabil Qabri, wa min adhaabin naari, wamin fitnatil mahyaa wal mamaati, wamin sharri fitnatil masiihiddajjaali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Allaahumma baaid bainiy -Ewe Mwenyezi Mungu weka mbali baina yangu- wa baina khatwaayaaya -na baina ya makosa yangu- kamaa baa a'tta bainal mashriqi wal maghribi -kama ulivyoweka mbali baina ya mashariki na magharibi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hivi nikuhadithieni hadithi kuhusu Dajali ambayo hajawahi kuhadithia Nabii yeyote watu wake! Hakika yeye ni chongo, na hakika atakuja akiwa pamoja na mfano wa pepo na moto,
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Linganeni sawa katika sijida, na asikunjue mmoja wenu mikono yake kama anavyokunjua mbwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilimuuliza Anas bin Malik: alikuwa Nabii Rehema na amani za Allah ziwe juu yake- akiswali na viatu vyake? akasema: ndio
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mtu huwa katika mwenendo wa rafiki yake wa karibu, basi na aangalie mmoja wenu ni nani anayemfanya kuwa rafiki yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Mfano wa rafiki mwema na rafiki muovu ni mfano wa mbeba miski na mfua vyuma
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Fanyeni haraka kufanya matendo kuna fitina nzito kama kipande cha usiku wa giza,
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake akisema mara kwa mara: “Ewe Mbadilishaji nyoyo, uweke imara moyo wangu katika dini yako.”
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakapokunywa mbwa katika chombo cha mmoja wenu basi akioshe mara saba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, ole wao waarabu na watahadhari dhidi ya shari iliyokaribia, imefunguliwa leo katika ngome ya Ya'juuju na Ma'ajuju upenyo wa kiasi hiki.”
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume Rehema na amani ziwe juu yake anapoingia msalani anasema: "Allaahumma inniy Auudhubika minal khubuthi wal khabaa ithi" (Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninajikinga kwako kutokana na mashetani wa kike na mashetani wa kiume)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake na haya zaidi kuliko hata bikira ndani ya chumba chake, basi anapoona jambo asilolipenda tunajua kuwa hapendi kwa kupitia usoni kwake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Muabuduni Mwenyezi Mungu peke yake msimshirikishe yeye na chochote, na acheni wanayosema baba zenu, na anatuamrisha swala na ukweli
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika utakuja kutokea uchoyo na kujipendelea baada yangu na mambo msiyoyajua (uzushi)" Wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu unatuamrisha nini? Akasema: "Mtekeleze haki ya wajibu kwenu, na mumuombe Allah haki yenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayemuomba Mwenyezi Mungu shahada (yaani kufa shahidi) kwa dhati, basi atamfikisha daraja ya mashahidi hata kama atafia juu ya godoro lake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Majaribio hayaachi kumpata muumini wa kiume na muumini wa kike katika nafsi yake, na watoto wake, na mali yake mpaka atakapokutana na Mwenyezi Mungu ilhali hana dhambi hata moja
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hana mja wangu muumini toka kwangu malipo yoyote pindi ninapomchukua kipenzi chake katika familia yake duniani kisha akasubiri (malipo mazuri) zaidi ya pepo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa safarini, akaswali swala ya ishaa ya mwisho, akasoma katika moja ya rakaa mbili kwa sura ya wattin wazzaitun, sijawahi kumsikia yeyote mwenye sauti nzuri au kisomo kizuri zaidi yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa anapo swali anatanua kati ya mikono yake mpaka unaonekana weupe wa kwapa zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Waliamrishwa watu kuwe kuagana kwao kwa mwisho ni katika nyumba (Alka'ba), isipokuwa likaondoshwa hilo kwa mwanamke mwenye hedhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Msiziombee mabaya nafsi zenu,wala msiwaombee vibaya watoto wenu,wala msiziombee vibaya mali zenu,nakhofia dua hizo zisikutane na muda ambao haombwi Mwenyezi Mungu katika muda huo chochote isipokuwa anakujibuni.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hujibiwa mmoja wenu anapokuwa hajafanya haraka: anasema: Nimemuomba Mola wangu, na wala sijaona ananijibu mimi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mahala pa karibu zaidi anapokuwa Mola Mlezi na mja ni katikati ya usiku wa mwisho
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hebu rudi kwa wazazi wako, na ukaishi nao vizuri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Dinari bora anayoitoa mtu: ni Dinari anayoitoa kwa familia yake, na dinari anayoitoa mtu kwa mnyama wake katika njia ya Mwenyezi Mungu, na dinari anayoitoa kwa watu wake katika njia ya Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakapoota mmoja wenu ndoto anayoipenda basi ndoto hiyo inatoka kwa Mwenyezi Mungu, hivyo, amshukuru Mwenyezi Mungu kwa ndoto hiyo na aisimulie, na akiota ndoto kinyume na hiyo katika yale anayoyachukia, basi ndoto hiyo inatokana na Shetani, basi aombe kinga kutokana na shari yake, na wala asiisimulie kwa yeyote, kwani haitomdhuru
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ajabu iliyoje ya jambo la muumini, hakika jambo lake lote ni kheri, na hakuna hilo kwa yeyote ila kwa muumini,
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna kwa baba yako matatizo baada ya leo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Namna ya kuoga janaba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume Rehema na amani ziwe juu yake anapooga kwa ajili ya janaba, anaosha mikono yake, na anatawadha udhu wake ule wa swala, kisha anaoga
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- anapopiga chafya anaweka mkono wake au nguo yake juu ya kinywa chake, na anapunguza sauti yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yalikuwa maneno ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ni maneno ya wazi anayaelewa kila mwenye kuyasikia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Je nisikuelezeni kwa kile ambacho ninakiogopea zaidi kwenu nyinyi kuliko hata masihi dajali? Wakasema: Tueleze ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, akasema: Ni shirki iliyofichikana, anasimama mtu kuswali anapendezesha swala yake kwakuwa anaona kuna mtu anamtazama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Msimfanyie Mwenyezi Mungu washirika na hali nyinyi mnajua, Amesema bin Abbas katika aya hii: Washirika, ni ushirikina, uliofichikana kuliko sauti ya mkanyago wa mdudu chungu katika jiwe kubwa jeusi katika giza nene la usiku.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mfano wa aliyesimama katika mipaka ya Mwenyezi Mungu na mwenye kuingia ndani yake, ni kama mfano wa watu waliotengeneza boti (safina)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Waelezeni watu yale wanayoyafahamu, Hivi mnataka akadhibishwe (apingwe) Mwenyezi Mungu na Mtume wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ataletwa mtu siku ya Kiyama, kisha atupwe motoni, ujiviringishe utumbo na vyote vilivyomo tumboni mwake, atazunguka nao (motoni) kama punda anavyozunguka na jiwe la kusagia nafaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Msilifanye kaburi langu kuwa sikukuu, wala nyumba zenu kuwa makaburi, na nitakieni rehma, kwani dua zenu hunifikia popote mlipo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilikuwa ni mtu mwenye kutokwa na madhii kwa wingi na nilikuwa nikiona haya kumuuliza Mtume Rehema na amani ziwe juu yake kutokana na nafasi ya binti yake kwangu, nikamuamrisha Mikidadi bin Aswadi, akamuuliza, akasema: "Aoshe tupu yake na atawadhe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Msiseme: Ni kwakutaka Mwenyezi Mungu na fulani, lakini semeni: Akitaka Mwenyezi Mungu kisha akataka fulani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
kuapa kwangu kwa jina la Mwenyezi Mungu kwa uongo napenda zaidi kuliko kuapa kwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu nikisema ukweli
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Hakika mtafuata njia za walio kuwa kabla yenu, hatua kwa hatua, na dhiraa kwa dhiraa,
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mtakapo vaa, na mtakapo tawadha, basi anzeni na kuliani kwenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakaye walea mabinti wawili mpaka wakafikia utu uzima atakuja siku ya Kiyama mimi na yeye (Namna hii)" Na akaviunganisha vidole vyake viwili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hamtoingia peponi mpaka muamini, na hamtoamini mpaka mpendane, je nisikufahamisheni juu ya jambo ambalo mkilifanya mtapendana? toleaneni salamu kwa wingi kati yenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Laiti nisingeliogopea uzito kwa waumini -au kwa umma wangu-; ningeliwaamrisha kupiga mswaki kila wakati wa swala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ni amali ipi inayopendeka zaidi kwa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Ni swala kwa wakati wake", Akasema: Kisha ipi? Akasema: "Kisha wema kwa wazazi wawili" Akasema: "Kisha ipi? "Akasema: "Kupigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hili ni jiwe lililotupwa Motoni muda wa (miaka) sabini iliyopita, na sasa linaanguka Motoni mpaka litafika katika kina chake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Amesimulia kuwa mtu mmoja alikula chakula kwa Mtume Rehema na amani ziwe juu yake kwa mkono wake wa kushoto, akasema: "Kula kwa mkono wako wa kulia", Akasema: Siwezi, akasema: "Kamwe, hutoweza!",
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayelingania katika uongofu, atakuwa kwake kapata malipo mfano wa malipo ya aliyemfuata, halipunguzi hilo chochote katika malipo yao
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ni nini kinachowaogopesha hawa? wanapatwa na ulaini (wanazikubali) katika aya zilizo wazi, na wanaangamia katika aya zinazotatiza
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna siku ambayo wanaamka ndani yake waja isipokuwa kuna Malaika wawili wanateremka, anasema mmoja wao: Ewe Mwenyezi Mungu mpe mtoaji badala, na anasema mwingine: Ewe Mwenyezi Mungu mpe mzuiaji (Bahili) hasara
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kuamini mikosi ni shirki, Kuamini mikosi ni shirki, Kuamini mikosi ni shirki, alisema hivyo mara tatu", Na hakuna yeyote miongoni mwetu isipokuwa ana chembe ya hilo, isipokuwa Mwenyezi Mungu huliondoa kwa kumtegemea
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Tukasema: Wewe ni bwana yetu, akasema: "Bwana ni Mwenyezi Mungu", Tukasema: Na mbora zaidi kuliko sisi katika fadhila, na mtoaji zaidi kuliko sisi, akasema: "Semeni kwa maneno mliyozoea, au baadhi yake, na wala asikukokoteni Shetani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nyanyua kichwa chako na sema yasikilizwe, na omba upewe, na taka utetezi utetewe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Enyi watu, tahadharini sana na kuchupa mipaka katika dini, kwani kilichowaangamiza waliokuwa kabla yenu ni kuchupa mpaka katika dini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilikuwa kwa Saidi bin Jubair akasema: Ni nani kati yenu aliyeiona nyota iliyodondoka jana usiku? Nikasema: Mimi, kisha nikasema: Ama mimi sikuwa katika swala, lakini niling'atwa (na Nge)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna kuambukizana, wala mikosi ya ndege, wala mkosi wa Bundi, wala mkosi wa Kipanga (Jamii ya ndege). Na mkimbie mwenye ukoma kama unavyomkimbia simba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hauondoi uchawi ila mchawi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ninamuapa Mwenyezi Mungu, ikiwa Mwenyezi Mungu atamuongoza mtu mmoja kupitia kwako, hilo ni bora zaidi kwako kuliko ngamia wekundu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe baba yangu mdogo, sema: Laa ilaaha illa llaahu (Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu) neno ambalo nitakutetea kwalo mbele ya Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Si chochote mbingu saba na ardhi saba katika kiganja cha Ar-Rahmaani -Mwingi wa rehema- isipokuwa ni kama punje ya ulezi katika mkono wa mmoja wenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Si chochote kursiy (Mahala anapoweka miguu Ar-Rahmani) katika Arshi isipokuwa ni kama bangili la chuma lililowekwa katika ardhi ya jangwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ni nani anayejiapiza kwangu kuwa sitomsamehe fulani? Hakika mimi nimemsamehe,na nimeyaporomosha matendo yako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna kuambukizana maradhi, wala kutuhumu mikosi kwa sababu ya ndege, na kinachonipendeza zaidi ni kujipa matumaini". Wakasema: Ni nini matumaini? Akasema: "Ni neno jema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakaye muandaa mpiganaji katika njia ya Mwenyezi Mungu basi na yeye atakuwa kapigana, na atakayemsimamia mpiganaji kwa wema katika familia yake basi na yeye atakuwa kapigana
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake Alisema kuhusu maanswari (watu wa Madina): Hawampendi ila mtu muumini, na hawamchukii ila mnafiki, atakayewapenda Answaar na Mwenyezi Mungu atampenda, na atakayewachukia Mwenyezi Mungu atamchukia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akiitembelea msikiti wa Qubaa kwa kipando na pia kwa miguu, anaswali ndani yake rakaa mbili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
akatawadha mbele yao udhu wa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Haitokei kuuliwa nafsi yoyote kwa dhulma isipokuwa hupata binadamu wa mwanzo fungu (la dhambi) kutoka katika damu hiyo, kwasababu yeye ndiye muanzilishi wa kwanza kuua.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hivi hukujua kuwa uislamu hufuta madhambi yaliyokuwa kabla yake, na kuwa kuhama kunafuta madhambi yaliyokuwa kabla yake, nakuwa Hija inafuta madhambi yaliyokuwa kabla yake?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilimjia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- naye akiwa anapiga mswaki kwa mswaki wa mti mbichi, Akasema: na ncha ya mswaki ikiwa katika ulimi wake, naye akisema: AAGH, AAGH (sauti ya kujigogoa), na mswaki ukiwa mdomoni mwake, kana kwamba anajigogoa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika ilikuwa inakutosheleza kupiga kwa mikono yako hivi" Kisha akapiga kwa mikono yake miwili chini ya ardhi mpigo mmoja, kisha ukapaka mkono wa kushoto juu ya mkono wa kulia, na juu ya viganja vyake na uso wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Fanyeni matendo na muwe na msimamo, na tambueni kuwa hatosalimika mmoja wenu kwa sababu ya matendo yake, wakasema: Hata wewe ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?! Akasema: Hata mimi isipokuwa atakaponifunika mimi Mwenyezi Mungu kwa huruma zake na fadhila zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika watu wakimuona dhalimu na wasimchukulie hatua, basi wako karibu Mwenyezi Mungu kuwaadhibu wote kwa adhabu yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilikuwa nikioga mimi na Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika chombo kimoja sisi wote tukiwa na janaba, na alikuwa akiniamrisha najifunga kikoi (kishida), ananigusa na mimi nikiwa katika hedhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika mja anaweza kuzungumza neno asilijali ndani yake akateleza kwa neno hilo nakuingia katika moto ambao umbali wake ni baina ya mashariki na magharibi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna Nabii aliyetumwa na Mwenyezi Mungu katika umma wowote kabla yangu, isipokuwa kunakuwa katika umma wake na watu wake wapendwa na watu wanaoyachukua mafundisho yake na wanafuata amri yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Aliingia Abdur Rahmani bin Abiibakari As swiddiq -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na mimi nikiwa nimemuegemeza kifuani kwangu, na Abdur Rahmani -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- akiwa na mswaki mbichi akisukutua nao, akauelekezea Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- macho yake-.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na mguu wake ukiwa tayari umeuweka kwenye kipandwa (yaani yuko tayari kwa safari): Ni jihadi ipi bora? Akasema: ni neno la haki kwa kiongozi muovu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nimepewa mambo matano ambavyo hakupewa mtu mwingine miongoni mwa Manabii kabla yangu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayesema: -Yaani: anapotoka nyumbani kwake-: Bismillaahi tawakkaltu a'la llaahi -kwa jina la Mwenyezi Mungu nimemtegemea Mwenyezi Mungu, Laa haulaa walaa quwwata illaa billaa- hakuna ujanja wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, huambiwa: Umeongozwa na umetoshelezwa na umekingwa, na shetani hujitenga mbali naye
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilimpa ahadi ya utiifu Mtume rehema na amani ziwe juu yake juu ya kushuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammad ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na kusimamisha swala, na kutoa zaka, na kusikia na kutii, na nasaha kwa kila muislamu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
usijekuacha mwisho wa kila swala kusema: Allaahumma ainni alaa dhikrika washukrika wahusni ibaadatika" Ewe Mwenyezi Mungu nisadie katika kukutaja na kukushukuru na kuzifanya vizuri ibada zako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mcheni na Allah Mola wenu Mlezi, na salini swala zenu tano, na fungeni mwezi wenu, na tekelezeni zaka zenu, na mtiini mwenye mamlaka kwenu, (Mkiyafanya haya) mtaingia pepo ya Mola wenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, hakika mtaamrisha mema, na mtakataza mabaya; au hakika atakuwa karibu zaidi Mwenyezi Mungu kukutumieni adhabu toka kwake, kisha mtamuomba na wala hamtojibiwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Adhabu kali ya moto itazipata nyayo za miguu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alichelewesha Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- swala ya ishaa, akatoka Omar, akasema: Swala Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, wamelala wanawake na watoto, akatoka na kichwa chake kikitona maji akisema: Lau kama nisingehofia kuwapa tabu umma wangu basi ningewaamrisha swala hii waiswali wakati huu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Amesema Mwenyezi Mungu: Kila amali ya mwanadamu hiyo ni ya kwake isipokuwa swaumu, bila shaka hiyo ni yangu na mimi ndiye ninayeilipa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakapokutana mmoja wenu na ndugu yake basi na amsalimie, ukiwatenganisha kati yao mti, au ukuta, au jiwe, kisha akakutana naye tena basi amsalimie tena
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Simama na uswali witiri ewe Aisha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mwenyezi Mungu ninajilinda kwa radhi zako kutokana na hasira zako, na salama yako dhidi ya adhabu zako, na ninajilinda kwako kutokana nawe, siwezi kuzidhibiti sifa zako kwa idadi maalum kama ambavyo wewe ulivyoisifu nafsi yako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Aliulizwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-: Ni swala ipi bora? Akasema: Ni kurefusha kisimamo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hivi nisikuelezeni watu wa peponi? Kila mnyonge mwenye kujishusha, na lau kama angeliapia kwa Mwenyezi Mungu basi angelimuepusha (na kutopokea kiapo chake), hivi nisikuelezeni watu wa motoni? kila jeuri mkaidi mwenye kiburi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Je! nikujulisheni mambo ambayo yakifanyika Allah hufuta madhambi na hupandisha daraja kwa mambo hayo?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Je, nisiwaambieni matendo bora zaidi kwenu, na masafi zaidi mbele ya Mfalme wenu, na yatakayo kunyanyueni juu zaidi katika daraja zenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika mimi ninajua neno ambalo lau kama angelisema yangemuondokea anayaoyapata (katika hasira), lau angesema: Audhubillaahi minash-shaitwani, -Najilinda kwa Mwenyezi Mungu kutokana na Shetani- ingemuondokea hasira anayoipata
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ndoto njema hutoka kwa Mwenyezi Mungu, na ndoto mbaya hutoka kwa Shetani, atakapoota mmoja wenu ndoto mbaya anayoiogopa basi na ateme kushotoni kwake, na aombe ulinzi kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shari zake, kwani ndoto hiyo haitomdhuru
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni kupi kunusurika? Akasema: "Shika ulimi wako, na ikutoshe nyumba yako, na lia kwa ajili ya makosa yako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika peponi kuna daraja mia moja kaziandaa Mwenyezi Mungu kwaajili ya wenye kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu kati ya daraja mbili ni kama masafa ya baina ya mbingu na ardhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mimi nipo katika dhana ya mja wangu kwangu, na Mimi nipo naye wakati anaponitaja
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilimuuliza Aisha, nikasema: Ni kwa jambo gani alikuwa akianza nalo Mtume rehema na amani ziwe juu yake anapoingia nyumbani kwake? Akasema: Kwa mswaki
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nijulishe juu ya amali ambayo nikiifanya nitaingia peponi. Akasema: "Umuabudu Mwenyezi Mungu na wala usimshirikishe na chochote, na usimamishe swala na utoe zaka ya wajibu, na ufunge mwezi wa ramadhani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Laiti Dunia ingelingana na ubawa wa mbu kwa thamani yake mbele ya Allah mtukufu basi kafiri asingekunywa fundo moja la maji.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kafaulu ikiwa atakuwa mkweli
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Siku bora zaidi iliyochomozewa jua ni siku ya Ijumaa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alitajwa kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake mtu mmoja aliyelala usiku mpaka pakapambazuka, akasema: "Huyo ni mtu aliyekojolewa na Shetani ndani ya masikio yake, au alisema: ndani ya sikio lake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ameangukia pua (kapata hasara), kisha Ameangukia pua (kapata hasara), kisha Ameangukia pua (kapata hasara), atakayewakuta wazazi wake wawili wakati wa utuuzima, mmoja wao au wote wawili, na akawa hakuingia peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Wamepata ushindi wenye kujitenga
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mambo kumi ni katika maumbile: Kupunguza masharubu, na kuziachia ndevu,na kupiga mswaki, na kupandisha maji puani, na kupunguza kucha, na kuosha fundo za vidole, na kunyofoa nywele za makwapani, na kunyoa nywele za sehemu za siri, na kustanji kwa maji.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Anafunga shetani juu ya kisogo cha kichwa cha mmoja wenu, pindi anapolala, mafundo matatu, anafunga katika kila fundo usiku kucha na husema : basi lala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Shikamana na kusujudu kwa wingi kwa ajili ya Allah, kwani hakika wewe huta sujudu kwa ajili ya Allah isipokuwa Allah atakupandisha kwa sijida hiyo daraja, na atakufutia kwa sijida hiyo makosa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Macho ya aina mbili hautoyagusa moto: Jicho lililolia kwa kumuogopa Mwenyezi Mungu, na jicho lililokesha likilinda kwaajili ya Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika kila umma una mtihani wake, na mtihani wa umma wangu: ni mali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akijitahidi katika siku kumi za mwisho, kwa namna ambayo hakujitahidi katika siku zingine
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Umma wangu wote unasamehewa isipokuwa wenye kutangaza wazi madhambi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Tulikuwa tukimuandalia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- mswaki wake na (maji yake kwaajili ya) twahara, basi Mwenyezi Mungu anamuamsha kwa muda anaotaka aamke nyakati za usiku, anapiga mswaki, na anatawadha na anaswali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika atakuja mtu mnene tena mkubwa siku ya kiyama akiwa halingani mbele ya Mwenyezi Mungu hata na uzito wa bawa la mbu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hatomsitiri mja mja mwenzie duniani isipokuwa Mwenyezi Mungu atamsitiri siku ya kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Asife mmoja wenu isipokuwa afe katika hali ya kumdhania vizuri Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilikutana na Ibrahimu usiku niliochukuliwa, Akasema: Ewe Muhammadi wafikishie umma wako salamu zangu, na uwaeleze kuwa pepo ina udongo mzuri, ina maji matam
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Haijabakia katika utume isipokuwa viashiria vya habari njema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Lau kama ningekuwa na dhahabu kubwa mfano wa mlima Uhudi, basi ningependa zisipite siku tatu nikiwa namiliki chochote katika mali hiyo zaidi ya kile ninachokihifadhi kwaajili ya kulipa madeni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ikiwa kama utakuwa kama ulivyosema, basi ni kana kwamba unawalisha majivu ya moto (dhambi wanazozipata ni kama mtu anayekula majivu ya moto), na bado anaendelea kuwa pamoja nawe msaidizi kutoka kwa Mwenyezi Mungu dhidi yao, madam bado uko katika hali hiyo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Haijawahi kupata vumbi miguu ya mja yeyote katika njia ya Mwenyezi Mungu, halafu ikaguswa na moto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Si chochote dunia katika Akhera isipokuwa ni kama mfano wa mmoja wenu anapoweka kidole chake baharini, kisha atazame kimerudi na nini?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna watu wowote watasimama katika kikao ambacho hawamtaji Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani yake, isipokuwa watanyanyuka mithili ya mzoga wa punda, na wanakua na majuto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Anachokipata aliyekufa shahidi katika maumivu ya kifo, ni kama maumivu anayoyapata mmoja wenu kutokana na kung'atwa na mdudu chungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hainifurahishi mimi kumiliki dhahabu mfano wa mlima huu wa Uhudi, zikapita siku tatu nikawa hata na dinari moja (katika mali hiyo) isipokuwa kiasi ninachokihifadhi kwaajili ya kulipa deni, isipokuwa niseme kwa waja wa Mwenyezi Mungu hivi na vile.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Tulikuwa kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake,inakaribia kama watu tisa au nane au saba hivi, akasema: "Hivi hamumpi ahadi ya utiifu Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?" Na tulikuwa bado wageni katika hilo, tukasema: Tumekwisha kupa ahadi ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, kisha akasema: "Hivi hamumpi ahadi ya utiifu Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?" Tukasema: tumekwisha kupa ahadi ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, kisha akasema: "Hivi hamumpi ahadi ya utiifu Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?" *Akasema: Tukanyoosha mikono yetu na tukasema: Tukasema: tumekwisha kupa ahadi ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu,........@
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mfano wa yule anayemtaja Mola wake na yule asiyemtaja Mola wake, ni mfano wa aliyehai na aliyekufa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika mimi ninakuhofieni baada yangu, yale mtakayofunguliwa juu yenu katika maua ya dunia na pambo lake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni nani mwenye haki zaidi ya kumfanyia wema wa karibu? akasema: mama yako, kisha mama yako kisha mama yako, kisha baba yako, kisha anayefuata kwa ukaribu kisha nayemfuata kwa ukaribu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayepatwa na umasikini akaushusha kwa watu hautozibwa umasikini wake, na atakayeushusha kwa Mwenyezi Mungu, basi ni karibu zaidi Mwenyezi Mungu kumpa riziki ya haraka au ya baadaye
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayetoa vitu vya namna mbili katika njia ya Mwenyezi Mungu huitwa katika milango ya pepo, ewe mja wa Mwenyezi Mungu hii ni kheri, atakayekuwa miongoni mwa watu wa swala ataitwa katika mlango wa swala, atakayekuwa katika watu wa jihadi ataitwa katika mlango wa jihadi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayeniona mimi ndotoni basi ataniona akiwa macho -au ni kana kwamba kaniona akiwa macho- hajifananishi shetani na mimi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayependa Mwenyezi Mungu amuokoe na Matatizo ya siku ya Kiyama, basi amtatulie shida mwenye hali ngumu au ampunguzie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayeswali (wakati) wa baridi mbili ataingia peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Muislamu atakapoulizwa kaburini anashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nimeamrishwa nipambane na watu mpaka washuhudie kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na wasimamishe swala, na watoe zaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika Mwenyezi Mungu ameniondolea mimi kwa umma wangu (madhambi ya) kukosea na kusahau, na yale waliyolazimishwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika mtu mwenye adhabu nafuu katika watu wa motoni ni yule atakayekuwa na viatu viwili na soli mbili vitokanavyo na moto, utakuwa ukitokota kwa hivyo ubongo wake kama kinavyotokota chungu, hatoona kuwa kuna yeyote mwenye adhabu kali kuliko yeye, kumbe yeye ndiye ana adhabu nafuu kuliko wote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hivi unaonaje ikiwa nitauwawa katika njia ya Mwenyezi Mungu, je yatafutwa makosa yangu?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alifariki Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hali yakuwa hakuna chochote nyumbani kwake anachoweza kukila mwenye ini (uhai) ila kiasi kidogo cha ngano kilichokuwa katika ubao wangu (wa kuhifadhia chakula), nikala mpaka kikakaa muda mrefu, nilipokipima kikamalizika
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yanamfuata maiti mambo matatu: familia yake na mali yake na matendo yake, vinarudi vitu viwili na kinabakia kimoja: wanarudi familia yake na mali yake, na yanabakia matendo yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atasogezwa muumini siku ya Kiyama karibu na Mola wake Mlezi Aliyetakasika na Kutukuka, kisha atamuwekea pazia lake, hapo atamuonyesha wazi madhambi yake ili akiri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Amsalimie aliyepanda anayetembea, na anayetembea aliyekaa, na wachache kwa wengi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
"Umeniuliza kuhusu jambo kubwa, lakini nijepesi kwa yule atakayefanyiwa wepesi na Mwenyezi Mungu Mtukufu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Wema ni tabia njema, na dhambi ni lile litakalokukereketa katika kifua chako, na ukachukia watu wasilione
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Enyi watu! Hakika Mwenyezi Mungu ni mzuri hakubali ila vizuri, na hakika Mwenyezi Mungu amewaamrisha waumini kwa yale aliyowaamrisha kwayo Manabii
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu ananyoosha mkono wake wakati wa usiku ili amsamehe mkosefu wa mchana, na ananyoosha mkono wake wakati wa mchana ili amsamehe mkosaji wa usiku, mpaka jua litakapochomoza kutoka magharibi yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Aliniusia mimi kipenzi changu -rehema na amani ziwe juu yake kwa mambo matatu: kufunga siku tatu katika kila mwezi, na rakaa mbili baada ya kuchomoza jua (Dhuhaa), na nisali witiri kabla sijalala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mtakapouona basi fungeni, na mtakapouona basi fungueni, ukifunikwa kwenu nyinyi basi ukadirieni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika katika yale waliyoyakuta watu miongoni mwa maneno ya kiutume ya mwanzo, usipokuwa na haya basi fanya ulitakalo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Acha linalokutia shaka fanya lisilokutia shaka, kwani ukweli ni utulivu, na bila shaka uongo ni shaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Swala ya mtu katika jamaa inazidi swala yake sokoni kwake na nyumbani kwake kwa daraja zaidi ya ishirini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kila kiungo kwa watu kina sadaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kuwa duniani kama msafiri au mpitanjia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ulimi wako usiache kuwa mbichi kwa kumtaja Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hawezi kuwa na imani mmoja wenu mpaka ampendelee ndugu yake anachokipenda yeye katika nafsi yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Laiti wangepewa watu yote wanayodai basi kuna watu wangedai mali za wenzao na damu zao, lakini ushahidi ni kwa mwenye kudai na kiapo ni kwa mwenye kukanusha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Usimuue, kwani ukimuuua basi yeye atakuwa katika nafasi yako kabla hujamuua, na wewe utakuwa katika nafasi yake kabla hajasema neno lake alilolisema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayekula kitunguusaumu, au kitunguu maji, basi na ajitenge nasi, au ajitenge na msikiti wetu, na akae nyumbani kwake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hautonyanyuka unyayo wa mja siku ya Kiyama mpaka aulizwe kuhusu umri wake aliumaliza katika mambo yapi? Na kuhusu elimu yake aliifanyia kazi katika nini? Na kuhusu mali yake ni wapi aliichuma? Na aliitoa katika mambo gani? Na kuhusu mwili wake aliumaliza katika mambo yapi?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika nitampa bendera hii mtu anayempenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake na Mwenyezi Mungu ataleta ufunguzi kupitia mikono yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hebu nielezeni lau kama Mto ungelikua mlangoni kwa mmoja wenu akioga humo kila siku mara tano, unasemaje kuhusu hilo, kunaweza kubaki na uchafu katika mwili wake?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu