عن عائشة رضي الله عنها قالت: «كان النبي صلى الله عليه وسلم يذكر الله على كل أحْيَانِه».
[صحيح] - [رواه مسلم والبخاري معلقا.
للفائدة: التعليق حذف الإسناد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Aisha- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: "Alikuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake akimtaja Mwenyezi Mungu katika nyakati zake zote".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy, ameiwekea maelezo kwa njia ya mkato
Maana ya hadithi: "Alikuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake akimtaja Mwenyezi Mungu" kwa aina zote za dhikiri miongoni mwa tasbihi- Yaani: Sub-haana llaah- na tahliil-Yaani: Laa ilaaha illa llah, na takbiir: Yaani Allahu Akbar, na Tahmidi: Yaani: Al-hamdulillah, na miongoni mwake ni kusoma Qur'ani; kwasababu Qur'ani ni katika dhikiri za Mwenyezi Mungu, bali yenyewe ndio aina bora ya dhikiri. "Katika nyakati zake zote" Yaani; Nikuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake alikuwa akimtaja Mwenyezi Mungu katika nyakati zake zote hata kama ana hadathi kubwa au ndogo (hana udhu), Ispokuwa wanachuoni wameondoa katika dhikiri za Mwenyezi Mungu Mtukufu kuisoma Qur'ani katika hali ya janaba, Mwenye janaba haruhusiwi kusoma Qur'ani moja kwa moja, si kwa kutazama wala moyoni; kwa mujibu wa hadithi ya Ally Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: "Alikuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake akitusomesha Qur'ani madamu tu hana janaba" Kaipokea Imam Ahmadi na wanachuoni wenye vitabu vya sunani vinne. Na wakatofautiana wanachuoni kwa mwenye hedhi na nifasi je, wanaunganishwa na mwenye janaba katika hukumu? Na kilicho wazi nikuwa inafaa kwao kusoma kwa moyo bila kugusa msahafu, kwasababu muda wao ni mrefu, na maamuzi hayako mikononi mwao kama mwenye janaba. Na pia inaondolewa katika kufaa kusoma Qur'ani katika hali yoyote: kuisoma wakati kukidhi haja ndogo au kubwa au wakati wa tendo la ndoa na katika maeneo ambayo hayaendani na utukufu wake, kama bafuni na chooni na maeneo mengine katika maeneo ya najisi.