+ -

عَنْ أَبِي ذَرٍّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّهُ سَمِعَ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ:
«لاَ يَرْمِي رَجُلٌ رَجُلًا بِالفُسُوقِ، وَلاَ يَرْمِيهِ بِالكُفْرِ، إِلَّا ارْتَدَّتْ عَلَيْهِ، إِنْ لَمْ يَكُنْ صَاحِبُهُ كَذَلِكَ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 6045]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Dharri radhi za Allah ziwe juu yake yakwamba yeye alimsikia Mtume rehema na amani ziwe juu yake akisema:
"Hatomtuhumu mtu mwenzake kwa machafu, na wala hatomtuhumu kwa ukafiri, isipokuwa hurejea kwake, ikiwa ndugu yake hatokuwa hivyo".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح البخاري - 6045]

Ufafanuzi

Ametahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa atakayesema kumwambia mwingine: Wewe ni muovu, au: Wewe ni kafiri, ikiwa hatokuwa kama alivyosema, basi yeye ndiye atakayestahiki sifa iliyotajwa, na kauli yake itarudi kwake, na ama akiwa kama alivyosema basi hakuna kitakachorejea kwake; kwa sababu atakuwa mkweli katika hayo aliyoyasema.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Pashto Kiassam الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Uharamu wa kuwatuhumu watu kwa ukafiri au uovu, pasina sababu ya kisheria.
  2. Ulazima kupata uhakika katika utoaji wa hukumu kwa watu.
  3. Amesema bin Daqiq Al-Iddi: Na hii ni tahadhari kubwa kwa atakayemkufurisha yeyote katika waislamu haliyakuwa hayuko hivyo, na huku ni kujitia mtegoni kukubwa.
  4. Amesema bin Hajari Al-Asqalaani: Lakini haipelekei kutokuwa kwake muovu au kafiri kutokupata dhambi katika sura ya kauli yake: Wewe ni muovu, bali katika sura hii kuna mchanganuo: Ikiwa atakusudia kumnasihi au kumnasihi mtu mwingine kwa kubainisha hali yake hapa itafaa, na ikiwa atakusudia kumuaibisha na kumtangaza kwa hilo na kumuudhi haitafaa; kwa sababu ameamrishwa na sheria kumsitiri na kumueleimisha na kumpa mawaidha kwa njia nzuri, kwa namna yoyote itakayowezekana kwake kuitumia kwa upole basi haifai kwake kutumia ukali; kwa sababu inaweza kuwa sababu ya kumhadaa na kumfanya aendelee na hilo, kama ilivyo tabia ya baadhi ya watu pale upole usipotumika, na hasa hasa atapokuwa muamrishaji yuko chini ya muamriwa katika cheo.