عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرِو بْنِ الْعَاصِ رضي الله عنهما قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«إِنَّ الْإِيمَانَ لَيَخْلَقُ فِي جَوْفِ أَحَدِكُمْ كَمَا يَخْلَقُ الثَّوْبُ الْخَلِقُ، فَاسْأَلُوا اللَّهَ أَنْ يُجَدِّدَ الْإِيمَانَ فِي قُلُوبِكُمْ».

[صحيح] - [رواه الحاكم والطبراني]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abdullahi Bin Umar -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na amani ziwe juu yake-:
"Hakika Imani huoza na kudhoofika kwenye mwili wa mmoja wenu kama inavyooza nguo mpya kwa kukaa muda mrefu, basi muombeni Mwenyezi Mungu aifanye Imani kuwa mpya kwenye nyoyo zenu."

Sahihi - Imepokelewa na Al Haakim

Ufafanuzi

Anatoa habari Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa Imani huoza katika moyo wa muislamu na inachakaa kama inavyochakaa nguo mpya kwa kutumika muda mrefu; Na kuoza huko ni kwa sababu ya udhaifu katika ibada, au kwa sababu ya kufanya maasi na kuzama kwenye matamanio. Basi anatoa muongozo Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- yakuwa tumuombe Mwenyezi Mungu Mtukufu azifanye kuwa mpya imani zetu, kwa kutekeleza mambo ya wajibu na kuzidisha kumtaja Mwenyezi Mungu na kumuomba msamaha.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Himizo la kumuomba Mwenyezi Mungu uimara na kuzifanya kuwa mpya imani katika nyoyo.
  2. Imani sahihi ni kauli matendo na itikadi, na imani inazidi kwa kutii, na hupungua kwa kufanya maasi.