عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «تعاهدوا هَذَا القُرْآنَ، فَوَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ لَهُوَ أشَدُّ تَفَلُّتاً مِنَ الإبلِ فِي عُقُلِهَا». .
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Musa Al-Ash'ariy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-: Amesema: "Shikamaneni na hii Qur'ani, Namuapia yule ambaye nafsi ya Muhammad iko mkononi mwake, hiyo ni nyepesi sana kuponyoka kuliko ngamia katika kamba zake".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
"Shikamaneni na Qur'ani": Yaani: Dumuni na kuisoma kwake, na mfululize katika kuisoma, na kauli yake: "Namuapia yule ambaye nafsi ya Muhammadi iko mkononi mwake hiyo ni nyepesi sana kuponyoka": Yaani kujiondoa, "kuliko hata ngamia katika kamba zake": Makusudio yake; ni kamba anayofungwa ngamia kati kati ya muundi, Ameifananisha Qur'ani kwa jinsi inavyohifadhiwa juu ya moyo na ngamia anayekimbia na hali yakuwa kafungwa na kamba, na Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa upole wake amewazawadia neema hii kubwa, hivyo inatakiwa washikamane nayo kwa kuihifadhi na kudumu nayo, akaiwekea kipande maalumu anachoshikamana nacho kila siku lazima akisome, ili asiisahau, ama atakayeisahau kiubinadamu basi hii haidhuru, lakini atakayeipuuza na akaghafilika nayo baada yakuwa Mwenyezi Mungu amemneemesha kuihifadhi, basi huyu anahofiwa huenda akaadhibiwa, ni lazima kuichunga Qur'ani kwa kushikamana nayo kwa kuisoma ili ibakie kifuani, na vile vile pia kwa kuifanyia kazi, kwasababu kuifanyia kazi hupelekea kuihifadhi na kuibakisha.