عن عثمان بن عفان رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «خَيرُكُم من تعلَّمَ القرآنَ وعلَّمَهُ».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Othmani bin A'ffani -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Mbora wenu ni yule aliyejifunza Qur'ani na akaifundisha".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

"Mbora wenu ni yule aliyejifunza Qur'ani na akaifundisha" Tamko hili linauhusu umma mzima, Mbora wa watu zaidi ni yule atakayekusanya kati ya sifa hizi mbili, atakayejifunza Qur'ani na akaifundisha Qur'ani, Akajifunza kwa mwingine naye akamfundisha mwingine; kwasababu kujifunza Qur'ani ni katika elimu tukufu, na kujifunza na kufundisha kunajumuisha kujifunza kwa lafudhi na maana, Atakayehifadhi Qur'ani yaani: akaanza kuwafundisha watu kisomo, na akawahifadhisha basi huyu anaingia katika kuifundisha, na vile vile atakayejifunza Qur'ani kwa namna hii basi na yeye anaingia katika kujifunza, Aina ya pili: kufundisha maana: Yaani: Kufundisha tafsiri, yaani mtu anakaa na watu anawafundisha tafsiri ya maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ni namna gani inatafsiriwa Qur'ani, mtu atakapomfundisha mwenzie namna gani afasiri Qur'ani na akampa kanuni katika hilo, basi huku ni katika kuifundisha Qur'ani

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa kujifunza Qur'ani tukufu na kuisoma vizuri, na ubora wa kuifundisha.
  2. Ubora wa kuyafanyia kazi yaliyomo miongoni mwa hukumu na adabu na tabia njema.
  3. Inampasa mjuzi kuitoa elimu baada ya kujifunza kwake.
  4. Kuthaminiwa mwenye kujifunza kitu katika Qur'ani, na kunyanyuliwa daraja yake kwa yale aliyojifunza.