Orodha ya Hadithi

Mfano wa waumini katika kupendana kwao na kuhurumiana kwao na kufanyiana kwao upole, ni kama mfano wa kiwiliwili, kinapopata tabu kiungo kimoja vinaitana kwa ajili ya hicho kimoja viungo vyote kwa kukesha na maumivu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Wasikilizeni na muwatii, kwani wao wana yao waliyobebeshwa nanyi mna yenu mliyobebeshwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Waamrisheni watoto wenu kuswali nao wakiwa watoto wa miaka saba, na wapigeni kwa ajili yake nao wakiwa watoto wa miaka kumi, na watenganisheni baina yao katika malazi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kumtukana Muislamu ni ufasiki (kutoka nje ya mipaka), na kupigana naye ni ukafiri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Msiwaanze Mayahudi wala wakristo kwa salam, mkikutana na mmoja wao njiani basi mbaneni mpaka adhikike
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna kitu chenye uzito zaidi katika mizani ya muumini siku ya Kiyama kuliko tabia njema, na hakika Mwenyezi Mungu anamchukia mtu muovu mwenye kauli chafu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika Mtume rehema na amani ziwe juu yake alitoka kwetu sisi, tukasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, tumekwishafahamu ni vipi tutakusalimu, sasa ni vipi tutakutakia Rehema?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hana swala yeyote ambaye hakusoma sura kifunguzi cha kitabu (suratul faatiha)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Si miongoni mwetu atakayepiga mashavu, na akachana mifuko, na akaomboleza kwa maombolezo ya watu wa zama za ujinga
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakaye koga siku ya Ijumaa josho la janaba, kisha akatoka katika saa ya kwanza ni kana kwamba katoa sadaka ya ngamia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayekuja miongoni mwenu kwa ajili ya Ijumaa basi na aoge
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Bahili ni yule ambaye nitatajwa mbele yake, akawa hakuniswalia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayekula chakula, akasema: Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu aliyenilisha chakula hiki, na akaniruzuku, si kwa ujanja wangu wala kwa nguvu zangu, atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayetawadha na akaufanya vizuri udhu, kisha akaja katika swala ya Ijumaa akasikiliza na akanyamaza atasamehewa yale yaliyoko kati ya Ijumaa yake hiyo na Ijumaa ijayo na ziada ya siku tatu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayekwenda asubuhi msikitini au mchana, Mwenyezi Mungu humuandalia nyumba peponi kila anapotoka asubuhi au jioni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Ewe mwanadam, maadamu unaniomba na kunitumainia, nitakusamehe uliyo nayo wala sitojali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Dua hairejeshwi (inayoombwa) baina ya adhana na kukimiwa swala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mwenyezi Mungu nitengenezee dini yangu ambayo ndiyo kinga ya jambo langu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mola wangu Mlezi nisamehe mimi makosa yangu, na ujinga wangu, na ubadhirifu wangu katika jambo langu lote, na yale unayoyajua kutoka kwangu, ewe Mola wangu nisamehe makosa yangu, na yale ya makusudi na ujinga wangu na mzaha wangu, na hayo yote yaliyo kwangu, ewe Mola wangu nisamehe niliyoyatanguliza na niliyoyachelewesha, na niliyoyaficha na niliyoyatangaza, wewe ndiye muwahishaji na wewe ndiye mcheleweshaji, na wewe juu ya kila kitu ni muweza
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba unipe afya katika Dunia na Akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba (unipe) kutoka katika heri zote: zile za haraka na za kuchelewa, kwa ninayo yajua na nisiyo yajua, na ninajikinga kwako kutokana na shari zote zinazokuja haraka na zinazochelewa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najikinga kwako kutokana na kuondokewa neema zako, na kubadilika kwa afya yako, na kufikiwa ghafla na adhabu zako, na kila aina ya hasira zako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninajikinga kwako kutokana na kushindwa kulipa deni, na kushindwa na maadui, na kutukanwa na maadui
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mwenyezi Mungu kwako tumeamka, na kwako tunashinda, na kwako tunakuwa hai, na kwako tutakufa, na kwako tutafufuliwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Muumini mwenye nguvu ni bora na anapendeka kwa Mwenyezi Mungu kuliko muumini dhaifu, na katika kila kheri,
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ilikuwa Dua aiombayo zaidi Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-:ni "Ewe Mola wetu Mlezi, tupe duniani mazuri, na Akhera mazuri, na utukinge na adhabu ya moto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Bwana wa Istighfari (Dua ya kuomba msamaha)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Enyi watu, toleaneni salamu na muunge udugu, na mlishe chakula, na msali usiku watu wakiwa wamelala, mtaingia peponi kwa amani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ogopeni dhulma, kwa hakika dhulma ni giza siku ya kiyama. Na ogopeni tamaa, kwa hakika tamaa iliwaangamiza walio kuwepo kabla yenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika dini ni nyepesi, na hatoifanyia mkazo dini yeyote ila itamshinda, basi shikamaneni na mfanye kadiri ya uwezo yanayoweza kukuwekeni karibu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ya kwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume rehema na amani zimfikie: Ni Uislamu upi bora? Akasema: "Ni, ulishe chakula, na utoe salamu kwa unayemjua na usiyemjua
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kila mmoja miongoni mwenu ni mchunga hivyo ataulizwa kuhusu raia wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Enyi kongamano la vijana mwenye uwezo miongoni mwenu wa kuoa na aoe, kwani ndoa ni sababu ya kuinamisha macho na kulinda tupu, na asiekuwa na uwezo basi ajilazimishe kufunga, hakika funga kwake itakata matamanio
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Tahadharini sana na kuingia/kukaa kwa wanawake" Mtu mmoja katika Maanswari akasema: Ewe Mtume wa Allah vipi kuhusu shemeji? Akasema: "Shemeji ni kifo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Fedha kwa dhahabu ni riba, ila kama itakuwa mkono kwa mkono, na ngano isiyokobolewa ni riba, ila kama itakuwa mkono kwa mkono, na shairi (ngano iliyokobolewa ni riba ila kama itakuwa mkono kwa mkono, na tende kwa tende ni riba ila kama itakuwa mkono kwa mkono
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Sema: Ewe Mwenyezi Mungu niongoze na unisimamie, na kumbuka kwa uongofu ni kuongoka kwako njia, na kusimamiwa ni kusimamiwa kupatia (katika kila jambo lako mithili ya) mshale
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake mtafuata nyenendo za wale waliokuwa kabla yenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba mtu mmoja alikuja kwa Mtume rehema na amani zimfikie, akamsemesha katika baadhi ya mambo, akasema: Akitaka Mwenyezi Mungu na ukataka, akasema Mtume rehema na amani zimfikie: "Umenifanya mimi kuwa mshirika wa Mwenyezi Mungu? sema: Akitaka Mwenyezi Mungu pekee
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Watu wenye adhabu kali zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu siku ya Kiyama, ni wale wenye kutengeneza mfano wa vile alivyoviumba Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Weka mkono wako juu ya mahala panapoumia katika mwili wako, na usema: Bismillaah, (kwa jina la Mwenyezi Mungu) mara tatu, na useme mara saba: Audhubillaahi wa quduratihi min sharri maa ajidu wa uhaadhiru (Ninajikinga kwa Mwenyezi Mungu na uwezo wake kutokana na shari ya kile ninachokipata na kile ninachokihofia)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Je, nisikujulisheni kitu bora zaidi kuliko hicho mlichoomba? Mtakapokwenda kulala basi msabihini Mwenyezi Mungu; yaani (Sub-haanallaah) mara thelathini na tatu, na mhimidini (Al-hamdulillaah) mara thelathini na tatu, na mtukuzeni (Allahu Akbar) mara thelathini na nne, kufanya hivyo ni bora zaidi kwenu kuliko mfanyakazi.”
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Sema Yeye ni Mwenyezi Mungu mmoja tu" na sura mbili za kinga unapofika nyakati za jioni na nyakati za asubuhi mara tatu, zitakutosheleza kila kitu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yeyote atakayesema: Bismillaahi lladhi laa yadhurru ma'asmihi shai un fil Ardhwi walaa fis samaai, wahuwas samiiu'l 'aliim, (Kwa jina la Mwenyezi Mungu ambaye hakuna kinachoweza kudhuru pamoja na jina lake kitu chochote ardhini wala mbinguni, naye ni msikivu na mjuzi) mara tatu, basi halitomfika balaa la ghafla, mpaka atakapoamka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Sema: Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiyekuwa na mshirika, Mwenyezi Mungu mkubwa mno, na kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu kwa wingi, na ametakasika Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu, na hapana ujanja wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu mwenye nguvu na hekima
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume wa Allah -rehema na amani ziwe juu yake ni mkarimu kuliko watu wote, na alikuwa mkarimu zaidi anapokuwa katika mwezi wa Ramadhani pindi anapokutana na Jibrili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kamwe, hatoingia motoni mtu yeyote aliyeswali kabla ya kuchomoza Jua na kabla ya kuzama kwake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna yeyote atakayenisalimia isipokuwa Mwenyezi Mungu hunirudishia roho yangu ili nimjibu salam
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna Muislamu yeyote atafikiwa na Sala ya lazima kisha akaufanya vizuri udhu wake, na Unyenyekevu wake na Rakaa zake, isipokuwa inakuwa ni kifuta madhambi yaliyo kuwa kabla ya Sala, kwa muda ambao hajafanya madhambi makubwa, na hivyo ndivyo ilivyo kila siku
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mfano wa muumini mwenye kusoma Qur'ani ni kama mfano wa chenza harufu yake nzuri na ladha yake nzuri, na mfano wa muumini ambaye hasomi Qur'ani ni kama mfano wa tende: haina harufu na ladha yake ni tamu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Adh-kari za baada ya sala ya faradhi hapati hasara msomaji au mfanyaji wake, kusema Sub-haana llahi mara thelathini na tatu (33), Al-hamdulillahi mara thelethini na tatu (33), Allahu Akbaru mara thelathini na nne (34)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayesema wakati anamsikia muadhini: Ninashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika nakuwa Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake, nimeridhia kuwa Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na Muhammadi kuwa ni Mtume na Uislamu kuwa ni dini, atasamehewa dhambi zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
kanipinga mwanadamu na hakustahiki kufanya hivyo, na amenitukana na hakustahiki kufanya hivyo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayemfanyia uadui kipenzi changu basi nitakuwa nimemtangazia vita, na hatojiweka karibu kwangu mja kwa kitu ninachokipenda katika vile nilivyomfaradhishia juu yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mambo mawili kwa watu hayo kwao ni ukafiri: Kutiana doa katika nasaba (ukoo), na kulia kwa kumuomboleza maiti
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakaye apa akasema katika kiapo chake: Na apa kwa Lata na uzza, basi aseme: Hapana apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na atakayesema kumwambia ndugu yake: Njoo tucheze kamari, basi na atoe sadaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Je mnajua ni nani aliyefilisika?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna mwenye kumiliki dhahabu wala fedha, na akawa hazitolei zaka zake, isipokuwa, pindi itakapofika siku ya Kiyama, atakunjiwa Sahani la kutoka motoni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna yeyote miongoni mwenu, isipokuwa ataongeleshwa na Mwenyezi Mungu siku ya Kiyama bila ya kuwapo na mkalimani yeyote kati yake na Yeye (Allah)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayetundika hirizi atakuwa kafanya ushirikina
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayesimulia kutoka kwangu mazungumzo ambayo yanaonekana kuwa ni uongo basi huyo ni mmoja kati ya waongo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
alikuwa anapoingia msikitini anasema: "Najilinda kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwa uso wake mkarimu, na kwa mamlaka yake ya tangu, kutokana na shetani aliyelaaniwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atanadi mwenye kunadi: "Hakika, mtapata afya nzuri na wala hamtougua milele. Na hakika, mtakuwa hai na wala hamtokufa milele, na hakika mtakuwa vijana na wala hamtazeeka milele. Na hakika, mtastareheka na wala hamtapata shida yoyote milele
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na Kutukuka, atawaambia watu wa Peponi: Enyi watu wa Peponi? Watasema: Labeka tumekuitikia na umetukuka, atasema: Je, mmeridhika? Watasema: Tuna nini mpaka tusiridhike hali yakuwa umetupa mambo ambayo hujampa yeyote katika viumbe wako?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Wakati wakazi wa Peponi watakapoingia Peponi, Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, atasema: "Je, mnataka kitu chochote niwazidishie?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ni safi Maji yake na ni halali mizoga yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Maji yatakapokuwa ni kulataini (Mapipa mawili) basi hayashiki uchafu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakapoamka mmoja wenu kutoka usingizini mwake basi na apenge kwa maji mara tatu, kwani Shetani hulala ndani ya tundu zake za pua
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba mtu mmoja alitawadha, akaacha sehemu ndogo saizi ya kucha miguuni kwake, akaiona Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake akasema: "Rudi katawadhe vizuri udhu wako" Akarudi, kisha akaswali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akiosha, au akioga, kwa kibaba kimoja mpaka vibaba vitano, na anatawadha kwa kibaba kimoja
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
“Hakuna Muislamu anayetawadha na akautia vizuri udhu wake, kisha akasimama na kuswali rakaa mbili, akielekea kwa moyo wake na uso wake ndani ya rakaa hizo, isipokuwa Pepo itastahiki kwake.”
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakapotawadha mmoja wenu na akavaa khofu zake (au soksi zake) basi na aswali nazo, na afute juu yake kisha asizivue akitaka kufanya hivyo isipokuwa atakapokuwa na janaba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hatomtuhumu mtu mwenzake kwa machafu, na wala hatomtuhumu kwa ukafiri, isipokuwa hurejea kwake, ikiwa ndugu yake hatokuwa hivyo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika shetani alishakata tamaa kuabudiwa na wenye kuswali katika kisiwa cha Arab, Lakini yuko katika kuwachochea baina yao
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Aina mbili za watu ni miongoni mwa watu wa motoni, sijawaona (katika zama zake Mtume), watu walio na mijeledi mithili ya mikia ya Ng'ombe wakiwapiga watu, na wanawake waliovaa na wako uchi, wanenguaji wakatikaji
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Asiangalie mwanaume katika uchi wa mwanaume mwenzie, wala mwanamke kutazama uchi wa mwanamke mwenzie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hawaingii Malaika nyumba ambayo ndani yake kuna mbwa au picha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hawafuatani Malaika na jamaa ambao ndani yao kuna mbwa au kengele
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Msiape kwa masanamu, wala kwa baba zenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayeiapia amana basi huyo si miongoni mwetu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Enyi hadhara ya wanawake, toeni sadaka, kwani hakika mimi nilionyeshwa kuwa nyinyi ndio wengi katika watu wa motoni" Wanawake wakasema: Na ni kwa nini ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Mnazidisha sana kulaani (kutukana) na mnawapinga waume, na mimi sijapata kuona wapungufu wa akili na dini wenye kuweza kuteka moyo ya mwanaume makini kuliko nyinyi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Tulikuwa hatuchukulii maji maji ya kahawia na njano baada ya twahara kuwa ni chochote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kaa kiasi cha siku ambazo ilikuwa ikidumu hedhi yako, kisha oga
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kuoga siku ya Ijumaa ni wajibu kwa kila aliyebaleghe, na apige mswaki, na aguse marashi ikiwa atapata
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nenda na viatu vyangu hivi viwili, yeyote utakayekutana naye mbele ya ukuta huu na hali yakuwa anashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu na moyo ukiwa na yakini kabisa na hilo, basi mpe habari njema kuwa yeye ni katika watu wa peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Muislamu wa kweli ni yule wanayepata Amani waislamu wenzake kutokana na ulimi wake na mkono wake, na mhamaji ni yule mwenye kuyahama yale aliyoyakataza Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Anayesoma Qur'ani kwa uhodari huwa pamoja na msafara wa Malaika watukufu, na anayesoma Qur'ani huku anasitasita na huku kwake bado ni ngumu huyo anamalipo mara mbili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Asisafiri mwanamke mwendo wa siku mbili mpaka awe pamoja na mume wake, au maharimu yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nyakati tatu alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akitukataza kuswali ndani yake, au kuzika ndani yake maiti wetu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayesema wakati anasikia adhana: Allaahumma rabba haadhihid da'watit taamma, was swalaatul qaaima, aati Muhammadanil wasiilata wal fadhwiila, wab'ath-huu maqaaman mahmuudanil ladhii wa a'ttah, (Ewe Mwenyezi Mungu, Mola wa wito huu uliotimia, na swala iliyosimama, mpe Muhammad utetezi na fadhila, na umfufue mahali pakusifiwa ulipomuahidi) basi utakuwa halali kwake utetezi wangu siku ya Kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Asiswali mmoja wenu katika nguo moja ambayo hakuna chochote mabegani mwake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hivi wana nini watu! wananyanyua macho yao mbinguni ndani ya swala zao", ikazidi ukali kauli yake katika hilo, mpaka akasema: "Hakika, ni ima waache kufanya hivyo, au yatapofuliwa macho yao
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Utakaposujudu basi weka viganja vyako, na unyanyue viwiko vyako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Niliswali pamoja na Mtume rehema na amani ziwe juu yake, alikuwa akitoa salaam kuliani kwake: "Assalaam alaikum warahamatullah wabarakaatuh", na kushotoni kwake: "Assalaam alaikum warahmatullah
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakaye msabihi Mwenyezi Mungu mwisho wa kila swala mara thelathini na tatu (33), na akamhimidi Mwenyezi Mungu mara thelathini na tatu (33), na akamtukuza Mwenyezi Mungu mara thelathini na tatu, hizo ni tisini na tisa (99) Na akasema ili kukamilisha mia moja (100): Laa ilaaha illa llaahu wahdahu laa shariika lahu, lahul Mulku walahul hamdu, wahuwaa'laa kulli shai in qadiir, basi yatasamehewa madhambi yake, hata kama yalikuwa na wingi mfano wa povu la Bahari
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yeyote atakayesoma Ayatul Kursiy mwisho wa kila swala ya faradhi hakuna kitakachomzuia kuingia peponi isipokuwa kufa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Msiwatukane Maswahaba wangu, kwa sababu, lau kama yeyote kati yenu atatoa dhahabu sawa na (mlima) Uhud (katika njia ya Mwenyezi Mungu), basi haiwezi kuwa sawa na theluthi mbili ya kilo ya mmoja wao wala nusu yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hatoingia motoni mtu aliyeshuhudia vita vya Badri na Hudaibia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alisema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- kumwambia Abubakari na Omari: "Hawa wawili ni mabosi wa watu wazima wa peponi kwanzia watu wa mwanzo na wa mwisho, isipokuwa Manabii na Mitume
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hassan na Hussein ni mabosi wa vijana wa peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika mmoja wenu anapokufa huonyeshwa makao yake asubuhi na jioni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Litafikia jambo hili ulipofika usiku na mchana, na wala hatoacha Mwenyezi Mungu nyumba ya mjini wala ya kijijini isipokuwa ataiingiza Mwenyezi Mungu dini hii
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakapopata shaka mmoja wenu katika swala yake, akawa hajui kaswali rakaa ngapi tatu au nne? Basi aachane na shaka na ajenge yakini (uhakika), kisha atasujudu sijida mbili kabla hajatoa salamu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake alikuwa haziachi rakaa nne kabla ya Adhuhuri na rakaa mbili kabla ya Alfajiri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayehifadhi rakaa nne kabla ya Adhuhuri na rakaa nne baada yake basi Mwenyezi Mungu atamharamisha kuingia motoni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake alisoma katika rakaa mbili za (sunna ya) Alfajiri {Qul yaa ayyuhal kaafiruun} na {Qul huwallaahu ahad}
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Imekuwa ni bora swala ya wengi kuliko swala ya mmoja wenu peke yake, kwa vipengele ishirini na tano, na hukusanyika Malaika wa usiku na Malaika wa mchana katika swala ya Alfajiri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Safu bora kwa wanaume ni safu ya kwanza, na safu yenye shari ni ya nyuma, na safu bora kwa wanawake ni safu ya mwisho na yenye shari ni safu ya mwanzo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake alimuona mtu mmoja akiswali peke yake nyuma ya safu, akamuamrisha arudie swala yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika swala hizi mbili, ni swala nzito sana kwa wanafiki, na lau kama mngejua malipo yaliyomo basi mngezijia, hata kwa kutambaa kwa magoti
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mwanamke yeyote atakayeolewa bila idhini ya walii wake, basi ndoa yake ni batili" Akasema hivyo mara tatu "Ikiwa atamuingilia basi mahari yake ndio itakuwa kwa ajili ya kile alichokifanya kwake, na ikiwa watazozona basi kiongozi ndiye msimamizi wa asiyekuwa na msimamizi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Amelaaniwa mwenye kumuingilia mke wake kinyume na maumbile
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hamtazami Mwenyezi Mungu mtu ambaye kamuingilia mwanaume au mwanamke katika tupu yake ya nyuma
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni zipi haki za mke wa mmoja wetu juu yake?, Akasema: "Ni umlishe pale unapokula, na umvishe unapovaa, au utakapopata kipato, na wala usipige uso, na wala usitoe maneno machafu, na wala usihame isipokuwa ndani ya nyumba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kamlaani Mtume rehema na amani ziwe juu yake mwenye kuunga nywele na mwenye kuungwa, na mwenye kuchora chata na mwenye kuchorwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayekuwa na wake wawili akaegemea kwa mmoja wao atakuja siku ya Kiyama upande wake mmoja ukiwa umepinda
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika Mwenyezi Mungu amewafutia umma wangu yale yanayozungumzwa na nafsi zao, madamu hayajafanyiwa kazi au kuzungumzwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Imenyanyuliwa kalamu kwa watu wa aina tatu: Kwa aliyelala mpaka aamke, na kwa mtoto mdogo mpaka abalehe, na kwa mwendawazimu mpaka apate akili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
kila kilevi ni haramu, na atakayekunywa pombe duniani na akafa akiwa mlevi kupindukia na hakutubia, hatoinywa huko akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Wapigeni vita washirikina kwa mali zenu na nafsi zenu na ndimi zenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, mimi sijaacha dhambi yoyote wala maasi yoyote isipokuwa nimeyafanya, akasema: "Hivi wewe hautamki neno la shahada "Ash-hadu an-laa ilaaha illa llahu wa anna Muhamadan rasuulullah?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
na hakika yeye hajawahi kusema hata siku moja: Ewe Mola wangu nisamehe makosa yangu siku ya Kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
"Hivi mnajua kuwa Mola wenu amesema nini?" Wakasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndiyo wanajua zaidi, akasema: "Watu wangu kwenye kuteremka Mvua wamegawanyika makundi mawili kuna waumini na makafiri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
kwa kusema kuwa hakika sisi twapata katika nafsi zetu mambo ambayo yamuia uzito mmoja wetu kuyasema, akasema: "Ni kweli mnayapata hayo kwenye nafsi zenu?" Wakasema: "Ndiyo" Akasema: "Hiyo ndiyo imani ya kweli
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mwenyezi Mungu ni mkubwa Mwenyezi Mungu ni mkubwa, namshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amevirudisha vitimbi vya Shetani na vikageuka kuwa ni wasiwasi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Shetani humjia mmoja wenu na akamwambia: Ni nani aliumba kitu fulani? Mpaka anafikia kusema ni nani alimuumba Mola wako? Basi ikiwa atafikia kuuliza hivyo basi na ajikinge kwa Mwenyezi Mungu na awache kuuliza maswali hayo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Matendo yapo ya aina sita na watu wapo wako aina nne, basi kuna watu wa aina mbili wanaostahiki malipo, na malipo yao huwa sawa na matendo yao, na jema moja hulipwa kwa kumi mfano wake, na jema moja huzidishwa mpaka kufikia mema mia saba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kwa hakika Mwenyezi Mungu hamdhulumu muumini kwa jema alilofanya, huandikiwa thawabu za wema wake hapa Duniani na hulipwa thawabu hizo huko Akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Umekwisha pokea malipo yako kutokana na mema uliyoyatanguliza
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kwa hakika Mwenyezi Mungu anapenda ichukuliwe ruhusa yake katika kufanya yaliyo mepesi, kama vile anavyopendelea kwa waja wake kufanya mambo yake aliyowawajibishia kuyafanya
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mfano wa mtu mnafiki, ni kama Mbuzi mwenye kutangatanga baina ya makundi mawili ya Mbuzi, wakati mwingine huwa na kundi hili na wakati mwingine huwa na kundi lile
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika Imani huoza na kudhoofika kwenye mwili wa mmoja wenu kama inavyooza nguo mpya kwa kukaa muda mrefu, basi muombeni Mwenyezi Mungu aifanye Imani kuwa mpya kwenye nyoyo zenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kwa hakika miongoni mwa alama za Kiyama ni kuondolewa elimu, na kuzidi ujinga, na kukithiri uzinifu, unywaji pombe, na wanaume watakuwa wachache na wanawake watakuwa wengi mpaka itafikia wanawake hamsini kusimamiwa na mwanaume mmoja
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakitosimama Kiyama mpaka apite mtu juu ya kaburi la mtu aseme: Natamani ningekua nafasi yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakitasimama Kiyama mpaka mpigane na Mayahudi, mpaka jiwe ambalo nyuma yake kuna Myahudi liseme: Ewe Muislamu huyu hapa Myahudi nyuma yangu njoo umuuwe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, hivi karibuni atakuteremkieni Issa mwana wa Mariam atakuwa hakimu na muadilifu, atavunja misalaba, na ataua nguruwe, na ataweka kodi (Jizia), na mali itabugujika (itakuwa nyingi) mpaka itafikia mahali hakuna yeyote atakayeikubali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakita simama Kiyama mpaka jua lichomoze kutoka upande wa Magharibi, na likichomoza na wakaliona watu wote wataamini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakitosimama kiyama mpaka zama zikaribiane
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ataikamata Mwenyezi Mungu ardhi, na ataikunja mbingu kwa mkono wake wa kulia kisha atasema: Mimi ndiye Mfalme; wako wapi wafalme wa ardhi?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Birika langu ukubwa wake ni sawa na mwendo wa mwezi mzima, maji yake ni meupe kuliko maziwa, na harufu yake ni nzuri kuliko ya Miski
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kwa hakika mimi nitakuwa kwenye Birika langu namtazama kila mwenye kuja kwangu kunywa, na kuna watu watafukuzwa, na nitasema: Ewe Mola wangu huyu anatokana na mimi na ni katika umma wangu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Namuapa yule ambaye nafsi yangu ipo mikononi mwake, kwa hakika vyombo vyake ni vingi kama wingi wa nyota mbinguni na sayari zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mauti yataletwa yakiwa kama dume la Kondoo mwenye rangi mchanganyiko ya weusi na weupe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Moto wenu wa Dunia ni sawa na sehemu tu ya sabini itokanayo na moto wa Jahannam
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ametuhadithia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- naye ni mkweli mwenye kukubaliwa: "Kwa hakika mmoja wenu hukusanywa umbile lake kwenye tumbo la mama yake mchana arobaini na nyusiku arobaini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kila jambo linakuwa kwa namna lilivyopangwa, mpaka kushindwa kufanya jambo fulani au kulifanya kwa ufanisi, au kufanya kwa ufanisi au kushindwa kabisa kufanya
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mwenyezi Mungu akimpangia mja afie sehemu fulani humfanya ahitajie kitu sehemu ile
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yeyote atakayenisingizia mimi uongo kwa makusudi basi ajiandalie makazi yake kuwa ni motoni
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
na mimi ndiye ninaitwa Dhwamam Bin Thaalaba ndugu wa Banii Saad Bin Bakri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alitaja jambo fulani, akasema: "Jambo lenye kuogopesha litakuwa wakati itakapo ondoka elimu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Msiwafanye Mayahudi na Manaswara kuwa ni wakweli wala ni waongo, na semeni hivi {Tumemuamini Mwenyezi Mungu na yote yaliyoteremshwa kwetu sisi}
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Msijifunze elimu kwa ajili ya kujifaharisha kuwa ni katika maulama, wala kwa kujadiliana na wasiokuwa na elimu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Amepigia mfano Mwenyezi Mungu wa njia iliyonyooka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Uliteremshwa Wahyi kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akiwa na umri wa miaka arobaini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, hajui kitenganishi kati ya Sura na Sura nyingine mpaka imteremkie {Bismillahir Rahmanir Rahiim}
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Je anapenda mmoja wenu pindi atakaporudi kwa mke wake apate Ngamia watatu wenye mimba na walio nenepa?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ataambiwa msomaji wa Qur'ani: Soma na upande daraja, na soma kwa utulivu kama ulivyokuwa ukisoma Duniani, kwa hakika upandaji wa cheo chako utakomea katika Aya ya mwisho utakayoisoma
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mwenye kuisoma Qur'ani kwa sauti ya wazi ni kama mwenye kutoa sadaka hadharani, na mwenye kuisoma Qur'ani kwa siri ni kama mwenye kuficha sadaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
walikuwa wakitusomea Aya kumi kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, hivyo hawakuwa wakichukua Aya kumi zingine mpaka wawe wamekwishayafanyia kazi yaliyo ndani ya aya hizo kumi kwa kujifunza na kuyafanyia kazi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe baba Mundhir, hivi unaijua aya gani katika kitabu cha Mwenyezi Mungu ambayo ni tukufu zaidi?" Akasema: Nikasema: {Allahu laa ilaaha illa huwal hayyul qayyuum} Al-baqara: Basi akanipiga katika kifua changu, akasema: Nakuombea Mwenyezi Mungu elimu ikupe furaha ewe baba Mundhir
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa anapolala kitandani kwake wakati wa kila usiku alikuwa akikusanya viganja vyake, kisha akivipuliza na kuvisomea : {Qul-huwallahu Ahad}, na {Qul-A uudhu birabbil falaq} na (Qul-Auudhu birabbi naas }
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mayahudi wameghadhibikiwa, na Wakristo ni wapotofu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ikiwa utawaona wenye kufuata Aya zenye kutatiza basi hao ndiyo ambao Mwenyezi Mungu amewataja katika aya
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakuna mtu yeyote atakayetenda dhambi, kisha akasimama akajitwaharisha, kisha akaswali, kisha akamuomba Allah msamaha, isipokuwa Mwenyezi Mungu humsamehe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Akasema: "Watahesabiwa kwa hiyana waliyokufanyia na kukuasi na kukudanganya, na itahesabiwa adhabu yako uliyowapa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hivi yule aliyemfanya atembee kwa miguu miwili hawezi kumfanya atembee kwa uso wake siku ya Kiyama?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Sema: Laa ilaaha illa llahu, nitakutolea ushuhuda wa kusilimu kwa maneno hayo siku ya Kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika haya unayoyasema na kuwalingania watu ni mambo mazuri, ikiwa utatwambia juu ya haya tuliyoyafanya kama yana kafara
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nenda kwamwambie: Wewe si miongoni mwa watu wa motoni, bali ni katika watu wa peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Enyi watu hakika Mwenyezi Mungu ameondosha kwenu nyinyi kiburi cha zama za ujinga, na kujifaharisha kwa nasaba
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kisha hakika bila shaka mtakuja kuulizwa kuhusu neema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kutakuwa mwisho wa umma wangu na watu, wakikuhadithieni mambo ambayo humkuwahi kuyasikia nyinyi wala baba zenu, ole wenu na ole wao
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Andika, namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, hakitoki ndani yake ila haki
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitawadha kila wakati wa swala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alitawadha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- mara moja moja
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Anasimulia kuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alitawadha mara mbili mbili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakapo hisi mmoja wenu chochote tumboni kwake, akapata wasi wasi, je kuna chochote kimemtoka au la?, basi asitoke msikitini mpaka asikie sauti, au anuse harufu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ni haki kwa kila muislamu aoge katika kila siku saba walau siku moja, aoshe ndani yake kichwa chake na mwili wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nilimwendea Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- nikitaka kuwa muislamu, akaniamrisha nioge kwa maji na mkunazi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mtakapo msikia muadhini basi semeni mfano wa yale anayo yasema, kisha mnitakie rehema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayejenga msikiti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu basi Mwenyezi Mungu atamjengea Peponi nyumba mfano wake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kusali ndani ya Msikiti wangu huu ni bora kuliko sala elfu moja zinazo swaliwa nje ya Msikiti huu isipokuwa Msikiti wa Makka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakapoingia mmoja wenu msikitini basi asali rakaa mbili kabla hajakaa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakapoingia mmoja wenu msikitini basi aseme: Allaahummaf-tah lii abwaaba rahmatika (Ewe Mola wangu, nifungulie milango ya rehema zako), na akitoka aseme: Allaahumma innii as-aluka min fadhlika (Ewe Mola wangu ninakuomba unipe katika fadhila zako)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ewe Bilali, simamisha swala, tupe raha kwayo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Enyi watu! Bila shaka nimefanya hivi ili muige na mjifunze swala yangu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Pindi mtakaposwali basi nyoosheni safu zenu, kisha akuongozeni mmoja wenu, atakapotoa takbira basi toeni takbira
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, hakika mimi ndiye mtu niliyekaribu zaidi kwenu nyinyi swala yangu kufanana na swala ya Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, bila shaka hii ndio ilikuwa swala yake mpaka alipoondoka duniani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mwizi mbaya zaidi kuliko watu wote, ni yule anayeiba swala yake" Akasema: Ataiba vipi swala yake? Akasema: "Hatimizi rukuu zake wala sijida zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- anaponyanyua mgongo wake kutoka katika rukuu anasema: "Sami'allaahu liman hamidah
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alikua akisema mwishoni mwa kila swala ya faradhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa akisema kati ya sijida mbiliL "Rabbigh-firlii, Rabbigh-firlii
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Huyo ni Shetani anaitwa Khinzab, ukimuhisi basi haraka sana taka ulinzi kutoka kwa Allah dhidi yake, na uteme kushotoni kwako mara tatu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika Mwenyezi Mungu hakubali amali yoyote isipokuwa ile itakayokuwa imetakasiwa nia, na ikakusudiwa kupata radhi za Allah (na kwenda kuuona uso wake)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Amekwisha ionja ladha ya imani, yule mwenye kumridhia Mwenyezi Mungu kuwa ndiye Mola wake, na Uislamu ndiyo dini, na Muhammad ni Mtume
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mambo manne yatakayekuwa kwake atakuwa mnafiki halisi, na itakayekuwa kwake sifa moja kati ya hizo, atakuwa na sifa ya unafiki mpaka aiache: Akizungumza husema uongo, na akiingia makubaliano hufanya hiyana, na akiahidi anakwenda kinyume, na akigombana huvuka mipaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Anapo kufa mwanadamu matendo yake hukatika isipokuwa mambo matatu: Sadaka yenye kuendelea, au elimu yenye manufaa, au mtoto mwema wa kumuombea dua
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiindonesia
Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika mama Sa'di amefariki, ni sadaka ipi bora ya kumfanyia? Akasema: "Maji" Akasema: tukachimba kisima, na akasema: Kisima hiki ni kwa ajili ya mama Sa'di
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiindonesia
Muumini si msemaji watu vibaya wala mtoaji wa laana wala muovu wala mwenye kauli chafu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayesema: (Laa ilaaha illa llahu, wah-dahu laa sharika lahu, Lahul mulku, Walahul hamdu, Wahuwa alaa kulli shaini Qadiir) kwa siku mara mia moja
عربي Lugha ya kiingereza Kibangali
Hakika majina yenu yanayopendeza zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni Abdullah na Abdul-Rahman
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiindonesia