عن أبي صرمة رضي الله عنه مرفوعاً: «من ضارَّ مسلما ضارَّه الله، ومن شاقَّ مسلما شقَّ الله عليه».
[حسن] - [رواه أبوداود والترمذي وابن ماجه وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Swarma Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Atakayemdhuru muislamu naye Mwenyezi Mungu atamdhuru, na atakayempa ugumu muislamu naye Mwenyezi Mungu atampa ugumu".
Ni nzuri - Imepokelewa na Ibnu Maajah

Ufafanuzi

Katika hadithi kuna uharamu wa kuudhi na kuingiza madhara na tabu kwa muislamu, sawa sawa hilo liwe katika mwili wake au familia yake au mali yake au watoto wake, nakuwa yeyote atakayeingiza madhara na tabu kwa muislamu basi Mwenyezi Mungu atamlipa kulingana na matendo yake, sawa sawa madhara hayo yawe ni kwa kumkosesha maslahi au kwa kutokea madhara kwa namna yoyote, na miongoni mwa huu uongo na udanganyifu katika miamala, ni kuficha mapungufu, na mtu kuchumbia juu ya uchumba wa ndugu yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Uharamu wa kumuudhi muislamu, kwa namna yoyote ile.
  2. Malipo huendana na matendo.
  3. Kuwalinda Mwenyezi Mungu waja wake waislamu, nakuwa yeye mwenyewe Mtukufu ndiye anaye watetea.