+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه أَنَّ رَسُولَ اللهِ صلَّى الله عليه وسلم قال:
«ما مِنْ أحَدٍ يُسلِّمُ علي إلا ردَّ اللهُ عليَّ رُوحي حتى أردَّ عليه السَّلامَ».

[إسناده حسن] - [رواه أبو داود وأحمد] - [سنن أبي داود: 2041]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake yakwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake amesema:
"Hakuna yeyote atakayenisalimia isipokuwa Mwenyezi Mungu hunirudishia roho yangu ili nimjibu salam".

[Upokezi wake ni mzuri] - [Imepokelewa na Abuu Daud - Imepokelewa na Ahmad] - [صحيح ابن حبان - 2041]

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa hurejeshewa roho yake ili ajibu salam kwa kila aliyemsalimia sawa sawa awe karibu au mbali; na maisha ya Akhera na kaburini ni jambo la ghaibu, hakuna ajuaye uhalisia wake isipokuwa Mwenyezi Mungu pekee, naye juu ya kila kitu ni muweza.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kikurdi Kihausa Kireno Kiassam الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Himizo la kukithirisha kumswalia na kumtakia amani Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
  2. Maisha ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika kaburi lake ni maisha kamili anayoishi mwanadam katika kaburi lake, hakuna awezaye kujua uhalisia wake ila Mwenyezi Mungu Mtukufu pekee.
  3. Hadithi hii si hoja kwa mtu anayesema kuwa Mtume rehema na mani ziwe juu yake yuko hai anaishi kama tunavyoishi sisi, tunasema hivi ili washirikina wasiitumie kama hoja ya kumtaka msaada Mtume rehema na amani ziwe juu yake, bali hayo ni maisha ya barzakh (kaburini).