عن أبي هريرة رضي الله عنه : أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «لا تجعلوا بيوتكم مَقَابر، إنَّ الشيطان يَنْفِرُ من البيت الذي تُقْرَأُ فيه سورةُ البقرة».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Yakwamba Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Msizifanye nyumba zenu kuwa makaburi, hakika shetani huikimbia nyumba ambayo husomwa ndani yake suratul Baqara".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Anaeleza Abuu Huraira- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakwamba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amekataza kuzifanya nyumba kuwa makaburi, zikawa mfano wa makaburi kwa kuacha kushughulika waliomo na swala na kusoma Qur'ani, Na hakika zimeitwa nyumba katika hali ya kutoswaliwa ndani yake kuwa ni makaburi; kwasababu haikubaliki swala makaburini, kisha akaeleza -Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa shetani anaikimbia nyumba ambayo wanasoma watu wake ndani yake suratul Baqara, kwa kukata kwake tamaa ya kuwashawishi na kuwapoteza kwasababu ya baraka za kisomo chake na kuyafanyia kwao kazi yaliyomo.