عن أبي هريرة رضي الله عنه : أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «لا تجعلوا بيوتكم مَقَابر، إنَّ الشيطان يَنْفِرُ من البيت الذي تُقْرَأُ فيه سورةُ البقرة».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Yakwamba Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Msizifanye nyumba zenu kuwa makaburi, hakika shetani huikimbia nyumba ambayo husomwa ndani yake suratul Baqara".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anaeleza Abuu Huraira- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakwamba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amekataza kuzifanya nyumba kuwa makaburi, zikawa mfano wa makaburi kwa kuacha kushughulika waliomo na swala na kusoma Qur'ani, Na hakika zimeitwa nyumba katika hali ya kutoswaliwa ndani yake kuwa ni makaburi; kwasababu haikubaliki swala makaburini, kisha akaeleza -Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa shetani anaikimbia nyumba ambayo wanasoma watu wake ndani yake suratul Baqara, kwa kukata kwake tamaa ya kuwashawishi na kuwapoteza kwasababu ya baraka za kisomo chake na kuyafanyia kwao kazi yaliyomo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kubainishwa kwa ubora wa suratul-Baqara.
  2. Shetani anaikimbia nyumba ambayo inasomwa ndani yake suratul-Baqara, na wala haisogelei.
  3. Haifai kuswali makaburini.
  4. Ni sunna kuzidisha ibada mbalimbali na swala za sunna katika majumba.