Aina ndogo

Orodha ya Hadithi

1. Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akipendezwa sana na kuanzia kulia, katika kuvaa kwake viatu, na kutana kwake nywele, na twahara yake, na katika mambo yake yote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
2. Mchungeni(mfuatilieni) Muhammadi -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa watu wa nyumba yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
3. Sikumuona Mtume -rehema amani ziwe juu yake- katu akipitiliza kucheka mpaka kionekane Kilimi ndani ya mdomo wake, bali alikuwa akitabasamu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
4. Msiziombee mabaya nafsi zenu,wala msiwaombee vibaya watoto wenu,wala msiziombee vibaya mali zenu,nakhofia dua hizo zisikutane na muda ambao haombwi Mwenyezi Mungu katika muda huo chochote isipokuwa anakujibuni.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
5. Atakapoota mmoja wenu ndoto anayoipenda basi ndoto hiyo inatoka kwa Mwenyezi Mungu, hivyo, amshukuru Mwenyezi Mungu kwa ndoto hiyo na aisimulie, na akiota ndoto kinyume na hiyo katika yale anayoyachukia, basi ndoto hiyo inatokana na Shetani, basi aombe kinga kutokana na shari yake, na wala asiisimulie kwa yeyote, kwani haitomdhuru
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
6. Atakaye walea mabinti wawili mpaka wakafikia utu uzima atakuja siku ya Kiyama mimi na yeye (Namna hii)" Na akaviunganisha vidole vyake viwili
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
7. Laiti nisingeliogopea uzito kwa waumini -au kwa umma wangu-; ningeliwaamrisha kupiga mswaki kila wakati wa swala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
8. Hakuna siku ambayo wanaamka ndani yake waja isipokuwa kuna Malaika wawili wanateremka, anasema mmoja wao: Ewe Mwenyezi Mungu mpe mtoaji badala, na anasema mwingine: Ewe Mwenyezi Mungu mpe mzuiaji (Bahili) hasara
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
9. Nilikuwa kwa Saidi bin Jubair akasema: Ni nani kati yenu aliyeiona nyota iliyodondoka jana usiku? Nikasema: Mimi, kisha nikasema: Ama mimi sikuwa katika swala, lakini niling'atwa (na Nge)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
10. Fanyeni matendo na muwe na msimamo, na tambueni kuwa hatosalimika mmoja wenu kwa sababu ya matendo yake, wakasema: Hata wewe ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?! Akasema: Hata mimi isipokuwa atakaponifunika mimi Mwenyezi Mungu kwa huruma zake na fadhila zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
11. Ewe Mwenyezi Mungu ninajilinda kwa radhi zako kutokana na hasira zako, na salama yako dhidi ya adhabu zako, na ninajilinda kwako kutokana nawe, siwezi kuzidhibiti sifa zako kwa idadi maalum kama ambavyo wewe ulivyoisifu nafsi yako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
12. Hivi nisikuelezeni watu wa peponi? Kila mnyonge mwenye kujishusha, na lau kama angeliapia kwa Mwenyezi Mungu basi angelimuepusha (na kutopokea kiapo chake), hivi nisikuelezeni watu wa motoni? kila jeuri mkaidi mwenye kiburi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
13. Hakika mimi ninajua neno ambalo lau kama angelisema yangemuondokea anayaoyapata (katika hasira), lau angesema: Audhubillaahi minash-shaitwani, -Najilinda kwa Mwenyezi Mungu kutokana na Shetani- ingemuondokea hasira anayoipata
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
14. Ndoto njema hutoka kwa Mwenyezi Mungu, na ndoto mbaya hutoka kwa Shetani, atakapoota mmoja wenu ndoto mbaya anayoiogopa basi na ateme kushotoni kwake, na aombe ulinzi kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shari zake, kwani ndoto hiyo haitomdhuru
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
15. Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni kupi kunusurika? Akasema: "Shika ulimi wako, na ikutoshe nyumba yako, na lia kwa ajili ya makosa yako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
16. Hakika peponi kuna daraja mia moja kaziandaa Mwenyezi Mungu kwaajili ya wenye kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu kati ya daraja mbili ni kama masafa ya baina ya mbingu na ardhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
17. Mimi nipo katika dhana ya mja wangu kwangu, na Mimi nipo naye wakati anaponitaja - 4 ملاحظة
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
18. Nilimuuliza Aisha, nikasema: Ni kwa jambo gani alikuwa akianza nalo Mtume rehema na amani ziwe juu yake anapoingia nyumbani kwake? Akasema: Kwa mswaki
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
19. Alitajwa kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake mtu mmoja aliyelala usiku mpaka pakapambazuka, akasema: "Huyo ni mtu aliyekojolewa na Shetani ndani ya masikio yake, au alisema: ndani ya sikio lake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
20. Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akijitahidi katika siku kumi za mwisho, kwa namna ambayo hakujitahidi katika siku zingine
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
21. Tulikuwa tukimuandalia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- mswaki wake na (maji yake kwaajili ya) twahara, basi Mwenyezi Mungu anamuamsha kwa muda anaotaka aamke nyakati za usiku, anapiga mswaki, na anatawadha na anaswali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
22. Hatomsitiri mja mja mwenzie duniani isipokuwa Mwenyezi Mungu atamsitiri siku ya kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
23. Asife mmoja wenu isipokuwa afe katika hali ya kumdhania vizuri Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
24. Ikiwa kama utakuwa kama ulivyosema, basi ni kana kwamba unawalisha majivu ya moto (dhambi wanazozipata ni kama mtu anayekula majivu ya moto), na bado anaendelea kuwa pamoja nawe msaidizi kutoka kwa Mwenyezi Mungu dhidi yao, madam bado uko katika hali hiyo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
25. Haijawahi kupata vumbi miguu ya mja yeyote katika njia ya Mwenyezi Mungu, halafu ikaguswa na moto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
26. Hakuna watu wowote watasimama katika kikao ambacho hawamtaji Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani yake, isipokuwa watanyanyuka mithili ya mzoga wa punda, na wanakua na majuto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
27. Mfano wa yule anayemtaja Mola wake na yule asiyemtaja Mola wake, ni mfano wa aliyehai na aliyekufa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
28. Hakika mimi ninakuhofieni baada yangu, yale mtakayofunguliwa juu yenu katika maua ya dunia na pambo lake - 2 ملاحظة
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
29. Atakayependa Mwenyezi Mungu amuokoe na Matatizo ya siku ya Kiyama, basi amtatulie shida mwenye hali ngumu au ampunguzie
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
30. Hakika mtu mwenye adhabu nafuu katika watu wa motoni ni yule atakayekuwa na viatu viwili na soli mbili vitokanavyo na moto, utakuwa ukitokota kwa hivyo ubongo wake kama kinavyotokota chungu, hatoona kuwa kuna yeyote mwenye adhabu kali kuliko yeye, kumbe yeye ndiye ana adhabu nafuu kuliko wote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
31. Atasogezwa muumini siku ya Kiyama karibu na Mola wake Mlezi Aliyetakasika na Kutukuka, kisha atamuwekea pazia lake, hapo atamuonyesha wazi madhambi yake ili akiri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
32. Wema ni tabia njema, na dhambi ni lile litakalokukereketa katika kifua chako, na ukachukia watu wasilione
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
33. Imenyanyuliwa kalamu kwa watu wa aina tatu: Kwa aliyelala mpaka aamke, na kwa mtoto mdogo mpaka abalehe, na kwa mwendawazimu mpaka apate akili - 2 ملاحظة
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
34. Atakayefunga siku moja katika njia ya Mwenyezi Mungu, atauweka mbali Mwenyezi Mungu uso wake na moto miaka sabini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
35. Wanaendelea watu kuwa katika kheri kwa muda wote watakaofanya haraka kufuturu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
36. Tulikuwa tukitoa kipindi alipokuwa nasi Mtume rehema na amani ziwe juu yake zakatul fitiri, kwa kila mdogo na mkubwa, huru au mamluki, kibaba cha chakula, au kibaba cha siyagi, au kibaba cha ngano, au kibaba cha zabibu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
37. Tulikula daku pamoja na Mtume rehema na amani ziwe juu yake, kisha akasimama kwenda katika swala, nikasema: Ulipita muda gani baina ya adhana na daku? Akasema: Kiasi cha (kusoma) aya hamsini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
38. Yakwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake alikuwa akikaa itikafu siku kumi za mwisho wa Ramadhani, mpaka alimpomfisha Mwenyezi Mungu, kisha wakakaa itikafu wake zake baada yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
39. Chelewesheni kula daku, hakika katika kuchelewesha kula daku kuna baraka - 2 ملاحظة
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
40. Msiitangulizie Ramadhani kwa swaumu ya siku moja wala siku mbili, isipokuwa mtu aliyekuwa akifunga swaumu fulani basi na aifunge
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
41. Alifaradhisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake zakatul-fitiri kibaba cha tende, au kibaba cha ngano, kwa mtumwa na aliyehuru, na mwanaume na mwanamke, na mdogo na mkubwa katika waislamu, na akaamrisha itolewe kabla ya watu kutoka kwenda katika swala
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
42. Si halali kwa mwanamke wa kiislamu kusafiri mwendo wa usiku mmoja, isipokuwa awe pamoja na mwanaume mwenye uharamu wa kumuoa (ndugu yake)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
43. Atakayesahau hali yakuwa kafunga akala au akanywa, basi atimize swaumu yake, kwani Mwenyezi Mungu kamlisha na kamnywesha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
44. Nilishuhudia swala ya Idd pamoja na Omari bin Khattwab radhi za Allah ziwe juu yake, akasema: Siku mbili hizi alikataza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kufunga ndani yake: Siku ya kufungua kwenu kutoka katika swaumu yenu, na siku nyingine ni ile mnayokula katika vichinjwa vyenu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
45. Nikuwa Talbiya (kuitika) kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kulikuwa ni: Labbaikallaahumma labbaika -Nimekuitikia ewe Mola nimekutikia, Labbaika laa shariika laka labbaika -Nimekuitikia huna mshirika wako nimekuitikia, Hakika sifa njema na neema zote ni zako pamoja na ufalme, wewe pekee usiye na mshirika
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
46. Utafuteni usiku wenye cheo (Lailatul Qadri) katika witiri za kumi la mwisho katika Ramadhani
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
47. Naona ndoto zenu zimeafikiana katika siku saba za mwisho, basi atakayetaka kuitafuta basi na aitafute katika siku saba za mwisho
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
48. Hivi kwani hajakuwekeeni Mwenyezi Mungu mambo mnayoweza kutoa sadaka: Hakika katika kila tasbihi (kauli ya sub-haanallaah) ni sadaka, na kila takbira (Allahu Akbaru) ni sadaka, na kila tahmidi (Alhamdulillah) ni sadaka, na kila tahalili (Laa ilaaha illallaahu) ni sadaka, na kuamrisha mema ni sadaka, na kukataza maovu ni sadaka, na katika kiungo cha siri cha mmoja wenu kuna sadaka
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
49. Atakayemtatulia muumini tatizo moja katika matatizo ya dunia, Mwenyezi Mungu atamtatulia yeye tatizo katika matatizo ya siku ya Kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
50. Enyi watu, tubieni kwa Mwenyezi Mungu, kwani mimi ninatubia kwa siku mara mia moja - 2 ملاحظة
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
51. hakika Mtume rehema na amani ziwe juu yake alijitenga mbali na mpiga mayowe, na mnyoa nywele, na mchana nguo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
52. Walikuwa wana wa Israeli wakiongozwa na Manabii, kila anapokufa nabii anafuatiwa na nabii mwingine, na hakika hakuna nabii baada yangu, na watafuata Makhalifa (viongozi) baada yangu, na watakithiri
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
53. Alikuwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- zinapoingia siku kumi (za mwisho wa ramadhani) anauhuisha usiku, na anawaamsha watu wake, na anaongeza juhudi na anakaza kikoi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
54. Kufanya ibada katika (nyakati) za vita vurugu na mauaji ni kama kuhama kuja kwangu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
55. Hakuna muislamu yeyote ataomba maombi yasiyokuwa ndani yake na kuomba dhambi wala kukata udugu, isipokuwa Allah atampa kwa maombi hayo moja kati ya mambo matatu: Moja ima amuharakishie maombi yake, au amlimbikizie ili amlipe siku ya Kiyama, au amuondoshee katika mabaya mfano wake" Wakasema: (Maswahaba) kwa hiyo tuzidishe? Akasema: "Allah ni mwenye kuzidisha mara dufu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
56. Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa akisema wakati wa matatizo: "Laa ilaaha illa llaahul a'dhwiimul haliim, Laa ilaaha illa llaahu Rabbul A'rshil A'dhwiim, Laa ilaaha illa llaahu Rabbu ssamaawaati warabbul A'rshil kariim" Tafsiri: Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mpole, Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Mola wa A'rshi tukufu, Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Mola wa mbingu, na Mola wa ardhi, na Mola wa A'rshi takatifu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
57. Hakuwahi kuswali tena Mtume rehema na amani ziwe juu yake swala yoyote baada kuteremka kwake: "Itakapokuja nusura ya Mwenyezi Mungu na ufunguzi" [An-Naswir:1] Isipokuwa alikuwa akisema ndani yake: "Sub-haanaka Rabbanaa wabihamdika Allaahummagh-firlii, (umetakasika Mola wetu Mlezi na sifa njema ni zako, ewe Mwenyezi Mungu nisamehe)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
58. Atakapopiga mwayo mmoja wenu basi na ashike mkono wake juu ya kinywa chake, kwani Shetani huingia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
59. Haki za muislamu juu ya muislamu mwenzake ni sita" Pakasemwa: Na ni zipi hizo ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?, akasema: "Ukikutana naye msalimie, na akikuita muitikie, na akikutaka nasaha mnasihi, na akipiga chafya akamhimidi Mwenyezi Mungu basi muombee dua ya rehema, na akiugua mtembelee, na akifariki msindikize - 4 ملاحظة
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
60. Hamtazami Mwenyezi Mungu mwenye kuburuza nguo yake kwa kiburi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
61. Atakayejikatia haki ya muislamu kwa mkono wake wa kulia, basi Mwenyezi Mungu atakuwa kamuwajibishia moto, na kamharamishia pepo" Bwana mmoja akamuuliza: Hata kikiwa kitu kidogo ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Hata kikiwa kijiti cha mswaki wa Araki
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
62. Neema mbili wamepoteza thamani yake watu wengi: Afya na wakati
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
63. Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa akisema katika sijida yake: "Ewe Mwenyezi Mungu nisamehe mimi dhambi zangu ndogo zake na kubwa zake za mwanzo wake na mwisho wake, za wazi zake na za siri zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
64. Hakika watoa laana hawatokuwa mashahidi wala watetezi siku ya Kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
65. Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenye haya Mkarimu, anamuonea haya mja wake atakapo nyanyua mikono yake kumuelekezea kisha amrejeshe patupu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
66. Hawajawahi kukaa watu kikao chochote wakawa hawakumtaja Mwenyezi Mungu ndani yake, na wala hawakumsalia Nabii wao, isipokuwa itakuwa ni hasara juu yao, akitaka atawaadhibu na akitaka atawasamehe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
67. Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akipendelea dua fupi yenye kukusanya, na anaacha mengine yasiyokuwa hiyo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
68. Kiapo hutoa bidhaa, na hufuta faida
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
69. Msiutukane upepo, mkiona yanayo kuchukizeni katika upepo basi semeni: Ewe Allah tunaomba kheri za upepo huu na kheri zilizomo, na kheri ambazo kwazo umeamrishwa upepo huu, na tunataka hifadhi na ulinzi kutokana na shari zake ,na shari ambazo kwa sababu yake umeamrishwa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
70. Asiseme mmoja wenu: Ewe Mwenyzi Mungu nisamehe ukitaka, nirehemu ukitaka, niruzukua ukitaka, na adhamirie maombi yake, kwani yeye anafanya ayatakayo, hakuna wa kumlazimisha
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
71. Amepata hasara mtu nitakayetajwa mbele yake na akawa hakunitakia rehema, na kapata hasara mtu ambaye itaingia Ramadhani mpaka ikatoweka kabla hajasamehewa, na kapata hasara mtu atakayewapata wazazi wake akiwa mtu mzima na wao wakiwa wazee na wakawa hawakumuingiza peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
72. Hana swaumu atakayefunga milele, na funga ya siku tatu ni sawa na kufunga mwaka mzima
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
73. "Wana nini watu waliosema kadhaa wa kadhaa? lakini mimi ninaswali na ninalala na ninafunga na ninakula, na ninaoa wanawake; atakayeuchukia muongozo wangu basi hayuko nami
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
74. Hakuna waislamu wawili watakaokutana wakapeana mikono isipokuwa watasamehewa kabla hawajaachana - 2 ملاحظة
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
75. Atakayehifadhi aya kumi za mwanzo wa suratul Kahf, atakingwa na Dajali". Na katika riwaya nyingine: "Za mwisho wa suratul Kahf
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
76. Atakayemtembelea mgonjwa ambaye hajafikiwa na mauti, akasema akiwa kwake mara saba: Namuomba Allah Mtukufu, Mola wa Arshi Tukufu, akuponye, isipokuwa Mwenyezi Mungu atamponya kwa maradhi hayo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
77. Hakika nyoyo za wanadamu zote ziko baina ya vidole viwili miongoni mwa vidole vya Rahmaan (Mwingi wa rehema), kama moyo wa mtu mmoja, anaugeuza kokote atakako
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
78. Hakuwahi kupewa hiyari Mtume rehema na amani ziwe juu yake baina ya mambo mawili hata siku moja isipokuwa atachukua jepesi lake, madamu si dhambi, ikiwa itakuwa ni dhambi, basi hujiwekanalo mbali kuliko watu wote
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
79. Allah amng'arishe mtu aliyesikia kutoka kwangu chochote akakifikisha kama alivyo sikia, huenda mfikishiwa akawa mwerevu zaidi kuliko aliye sikia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
80. Mwenyezi Mungu atawakusanya watu wa mwanzo na mwisho katika udongo mmoja, atawasikilizisha mwenye kunadi, na atawapa upeo wa kuona, na jua linaposogea, watu watafikwa na tabu na matatizo kiasi ambacho hawatoweza kuvumilia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
81. Hakika muumini peponi atakuwa na Hema moja la madini ya lulu lililo wazi urefu wake kwenda juu ni maili sitini, muumini humo atakuwa na wake, akiwazungukia na wala baadhi yao hawawaoni wenzao
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
82. Amemlaani Mtume rehema na amani ziwe juu yake mwanaume anayevaa vazi la mwanamke, na mwanamke anayevaa vazi la mwanaume
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
83. Atakayeandaa mnyama kwa ajili ya kuchinja, na ukaandama mwandamo wa mwezi Dhul Hija, basi asipunguze chochote katika nywele zake wala kucha zake mpaka atakapochinja mnyama wake wa Udh-hiya
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
84. Inapokuja Ramadhani hufunguliwa milango ya pepo na hufungwa milango ya moto, na mashetani hufungwa minyororo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu