عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بنٍ مسعُودٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ:

ذُكِرَ عِنْدَ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ رَجُلٌ نَامَ لَيْلَهُ حَتَّى أَصْبَحَ، قَالَ: «ذَاكَ رَجُلٌ بَالَ الشَّيْطَانُ فِي أُذُنَيْهِ، أَوْ قَالَ: فِي أُذُنِهِ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa bin Mas'udi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Alitajwa mbele ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- mtu aliyelala usiku mpaka pakapambazuka, Akasema: "Huyo mtu kamkojolea shetani masikioni mwake, au alisema: sikioni kwake".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Maana ya hadithi: Anasema bin Mas'udi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: "Alitajwa mbele ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- mtu aliyelala usiku mpaka pakapambazuka", Yaani aliendelea kulala na wala hakuamka kusali kisimamo cha usiku, mpaka ikamchomozea alfajiri, Na kauli ya pili: Nikuwa yeye hakuamka kwaajili ya swala ya alfajiri mpaka jua likachomoza. Akasema: "Huyo mtu kamkojolea shetani masikioni mwake" na kauli hii iko kama ilivyo na inabaki katika uhalisia wake; kwasababu imethibiti kuwa shetani anakula na anakunywa na anaoa, Hivyo hakuna kinachozuia asikojoe, na huku ni kumdhalilisha kumfedhehesha kuliko pita kiasi, kuwa shetani kamfanya kuwa choo. Na ametaja masikio pekee pamoja nakuwa jicho ndiyo lilistahiki zaidi kwakuwa hulala ikiwa kama ni ishara ya uzito wa usinginzi, kwasababu masikio ndiyo vyanzo vya kuwa macho na ametaja mkojo pekee; kwasababu ndiyo mwepesi kupenya sehemu zilizo wazi na ni mwepesi kupita katika mishipa ukazalisha uvivu katika viungo vyote.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama

Maana ya Maneno