+ -

عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم:
«إِذَا مَرِضَ الْعَبْدُ أَوْ سَافَرَ كُتِبَ لَهُ مِثْلُ مَا كَانَ يَعْمَلُ مُقِيمًا صَحِيحًا».

[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 2996]
المزيــد ...

Imepokelewa Kutoka kwa Abuu Musa Al-Ash'ariy -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-:
"Pindi anapougua mja au akasafiri basi huandikiwa mfano wa yale aliyokuwa akiyafanya akiwa nyumbani tena mwenye afya".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [صحيح البخاري - 2996]

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuhusu fadhila za Allah na rehema zake, nakuwa muislamu ikiwa ni katika mazoea yake kufanya matendo mema akiwa katika hali ya afya na yuko nyumbani, kisha apatwa na udhuru akaugua akashindwa kutekeleza ibada hizo, au akashughulishwa na safari, au udhuru wowote; basi huandikiwa malipo kamili, kama ambavyo angefanya wakati wa afya na yuko nyumbani.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية Luqadda qer-qeesiya النيبالية Luqadda yuruuba الليتوانية الدرية الصومالية الطاجيكية Luqadda kiniya ruwadiga الرومانية المجرية التشيكية Luqadda malgaashka Kiitaliano Luqadda Oromaha Luqadda kinaadiga Luqadda Asariga الأوزبكية الأوكرانية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Upana wa fadhila za Allah kwa waja wake.
  2. Himizo la kuongeza juhudi katika ibada na kutumia fursa ya nyakati za afya na wasaa.