+ -

عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم:
«مَنْ يُرِدِ اللهُ بِهِ خَيْرًا يُصِبْ مِنْهُ».

[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 5645]
المزيــد ...

Imepokewa Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-:
"Mwenye kutakiwa kheri na Allah, (Allah) humuonja kutokana na kheri hiyo.

[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [صحيح البخاري - 5645]

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehama na amani ziwe juu yake- yakuwa Mwenyezi Mungu akitaka kheri kwa yeyote katika waja wake waumini huwapa mtihani katika nafsi zao na mali zao, na familia zao, kwa kile kinachotokea kwa muumini ikiwemo kurejea kwa Allah Mtukufu kwa maombi na dua, na kufutiwa makosa, na kunyanyuliwa daraja.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية Luqadda qer-qeesiya النيبالية Luqadda yuruuba الليتوانية الدرية الصربية الصومالية الطاجيكية Luqadda kiniya ruwadiga الرومانية المجرية التشيكية Luqadda malgaashka Kiitaliano Luqadda Oromaha Luqadda kinaadiga Luqadda Asariga الأوزبكية الأوكرانية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa muumini anakabiliwa na mabalaa mbali mbali.
  2. Mtihani unaweza kuwa alama ya mapenzi ya Allah kwa mja wake, ili amnyanyue daraja yake, na ampandishe cheo chake, na amfutie madhambi yake.
  3. Himizo la kuwa na subira wakati wa matatizo na kutolalama.