«لَا تَقُولُوا: مَا شَاءَ اللهُ وَشَاءَ فُلَانٌ، وَلَكِنْ قُولُوا: مَا شَاءَ اللهُ ثُمَّ شَاءَ فُلَانٌ».
[صحيح بمجموع طرقه] - [رواه أبو داود والنسائي في الكبرى وأحمد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Hudhaifa bin Yamani -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Msiseme: Ni matakwa ya Mwenyezi Mungu na matakwa ya fulani, lakini semeni: Ni matakwa ya Mwenyezi Mungu kisha akataka fulani".
Sahihi - Imepokelewa na An-Nasaaiy
Anakataza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuunganishwa jina la kiumbe kwa kiunganishi cha (wau yaani; Na) baada ya kutaja matashi na mfano wake; kwasababu anayeunganishwa hapo atakuwa kalingana sawa na yule aliyeunganishwa naye; ni kwasababu ima kiliwekwa kiunganishi hiki kwasababu ya kuvijumuisha vitu pamoja, hivyo ikawa hakimaanishi mpagilio wala kutanguliza kimoja baada ya kingine; na kumlinganisha muumba na kiumbe ni shirki, na anaruhusu Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kumuunganisha kiumbe na muumba kwa kutumia kiunganishi (Kisha); kwasababu hapa anayeunganishwa anakuwa kacheleweshwa na katengwa mbali na aliyeunganishwa naye kwa kidogo, hapa hakuna katazo; kwasababu hapa anakuwa yeye kafuatia (kaja baada).