عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه أَنَّ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«لَا تَصْحَبُ الْمَلَائِكَةُ رُفْقَةً فِيهَا كَلْبٌ وَلَا جَرَسٌ».

[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Hawafuatani Malaika na jamaa ambao ndani yao kuna mbwa au kengele".

Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa Malaika hawafuatani na msafara katika safari, na ndani ya msafara kuna mbwa, au kengele inayotundikwa kwa wanyama ikitoa sauti mnyama anapotembea.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Katazo la kufuga mbwa na kusuhubiana nao, isipokuwa mbwa wa kuwinda au wa ulinzi.
  2. Malaika wanaojizuia kufuatana na msafara ni Malaika wa rehema, ama wale waandika matendo hao hawamwachi mtu akiwa nyumbani au safarini.
  3. Katazo la kengele; kwani ni zumari katika mazumari ya shetani, na kuna kujifananisha na Wakristo.
  4. Ni juu ya muislamu kujiweka mbali na yale yote yanayowaweka Malaika mbali naye .