عن عبد الله ابن عباس رضي الله عنهما مرفوعاً: «إن الله تَجَاوزَ لِي عن أمتي الخطأَ والنِّسْيانَ وما اسْتُكْرِهُوا عليه».
[صحيح لطرقه] - [رواه ابن ماجه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillah bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika Mwenyezi Mungu ameniondolea mimi kwa umma wangu (madhambi ya) kukosea na kusahau, na yale waliyolazimishwa".
Ni sahihi kwa njia zake na ushahidi wake - Imepokelewa na Ibnu Maajah

Ufafanuzi

Miongoni mwa huruma ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa umma huu ni kuusamehe madhambi ya kukosea -Nayo ni yale ambayo hawajakusudia miongoni mwa maasi- na kusahau wajibu wao au kufanya maharamisho, lakini baadaye akikumbuka wajibu wake anaufanya, hivyo hivyo hata yale waliyolazimishwa na wakatezwa nguvu kuyafanya katika maasi na makosa ya jinai, Akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na hakukufanyieni juu yenu uzito katika dini".

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama