«إِذَا لَقِيَ أَحَدُكُمْ أَخَاهُ فَلْيُسَلِّمْ عَلَيْهِ، فَإِنْ حَالَتْ بَيْنَهُمَا شَجَرَةٌ أَوْ جِدَارٌ أَوْ حَجَرٌ ثُمَّ لَقِيَهُ فَلْيُسَلِّمْ عَلَيْهِ أَيْضًا».
[صحيح] - [رواه أبو داود]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakapokutana mmoja wenu na ndugu yake basi na amsalimie, ukiwatenganisha kati yao mti, au ukuta, au jiwe, kisha akakutana naye tena basi amsalimie".
Sahihi - Imepokelewa na Abuu Daud
Muislamu ameamrishwa kwa njia ya kumpendezeshea kutoa salamu kwa ndugu yake muislamu kila anapokutana naye, hata kama wakiwa pamoja, kisha wakaachana kwa lengo miongoni mwa malengo, kisha wakakutana tena, hata kama ni muda kidogo, basi katika mafundisho ni amsalimie na wala asiseme: mimi nilikuwa naye hivi karibuni, bali amsalimie, hata kama utawatenganisha kati yao mti, au ukuta, au jiwe kiasi ambacho atatoweka machoni mwake, basi katika mafundisho anapokutana naye mara ya pili ni amsalimie.