Hadithi: Hakika dunia ni tamu, ni ya kijani, na hakika Mwenyezi Mungu anakumilikisheni ndani yake aone ni namna gani mtafanya, iogopeni dunia na waogopeni wanawake
imepokewaKutoka kwa Abii Saidi Al-Khudry radhi za Allah ziwe juu yake kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Hakika dunia ni tamu, ni ya kijani, na hakika Mwenyezi Mungu anakumilikisheni ndani yake aone ni namna gani mtafanya, iogopeni dunia na waogopeni wanawake, kwani hakika fitina ya kwanza ya wana wa Israeli ilikuwa kwa wanawake"
الملاحظة
Uiu
النص المقترح Ikhhuy678yhbkii7uudc
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 2742]Ufafanuzi
Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa Dunia ina ladha tamu, na ni kijani katika mandhari, hivyo mwanadamu hudanganyika nayo na kuikimbilia na kuifanya kuwa ndio hamu yake kubwa. Nakuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu amewafanya baadhi yetu kuwa warithi wa wengine katika dunia hii, ili aone ni namna gani tutafanya, je tutasimama katika utiifu wake, au maasi yake? Kisha akasema: Tahadharini sana na zisikudanganyeni starehe za Dunia na mapambo yake, zikakupelekeeni kuacha aliyokuamrisheni Mwenyezi Mungu, na kuingia katika yale aliyokukatazeni. Na miongoni mwa mambo makubwa ya wajibu kutahadhari nayo katika fitina za Dunia ni fitina ya wanawake, nakuwa ndio iliyokuwa fitina ya kwanza waliotumbukia ndani yake wana wa Israeli.
Katika Faida za Hadithi
Himizo la kushikamana na uchamungu, na kutojishughulisha na mambo ya kidunia na pambo lake.
Tahadhari ya kufitinika na wanawake, kwa kuwatazama au kujiachia kwa kuchanganyika na wanaume wa kando, au mengineyo.
Fitina ya wanawake ni katika fitina kubwa katika Dunia.
Kuzingatia na kuchukua mafunzo kutoka katika umma zilizotangulia, kilichotokea kwa wana wa Israeli kinaweza kutokea kwa wengine pia.
Fitina ya wanawake, akiwa ni mke anaweza kumbebesha mwanaume mzigo mkubwa wa matumizi asiouweza, na akamshughulisha na kutafuta mambo ya kidunia, na akampelekea kumaliza umri wake katika kuitafuta Dunia, na akiwa ni mwanamke wa kando, anaweza kumfitini kwa kumlaghai mwanaume na kumtoa katika haki pale wanawake wakitoka na kuchanganyika pamoja na wanaume, hasa hasa wakiwa hawajisitiri kisheria, na hili linaweza kupelekea kuingia katika zinaa kwa ngazi zake, hivyo ni lazima kwa muumini kujikinga kwa Mwenyezi Mungu, na kuelekea kwake ili kusalimika na fitina za zao.
Tafsiri:Lugha ya kiingerezaLugha ya KiurduKiispaniaLugha ya KiindonesiaKi ighoriKibangaliLugha ya kifaransaKiturukiLugha ya KirashiaLugha ya KibosniaKisin-halaKihindiKichinaKifursiKivetenamuKitagalogiKikurdiKihausaKirenoKimalayoKitelguuKunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiriBurmeseGermanPashtoKiassamAlbanianالسويديةالأمهريةالهولنديةالغوجاراتيةLuqadda qer-qeesiyaالنيباليةLuqadda yuruubaالليتوانيةالدريةالصربيةالصوماليةLuqadda kiniya ruwadigaالرومانيةالمجريةالتشيكيةالموريLuqadda malgaashkaLuqadda OromahaLuqadda kinaadigaالولوفLuqadda Asarigaالأوكرانيةالجورجيةالمقدونية
+Ufafanuzi+Lugha ya kiingereza+Lugha ya Kiurdu+Kiispania+Lugha ya Kiindonesia+Ki ighori+Kibangali+Lugha ya kifaransa+Kituruki+Lugha ya Kirashia+Lugha ya Kibosnia+Kisin-hala+Kihindi+Kichina+Kifursi+Kivetenamu+Kitagalogi+Kikurdi+Kihausa+Kireno+Kimalayo+Kitelguu+Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri+Burmese+German+Pashto+Kiassam+Albanian+السويدية+الأمهرية+الهولندية+الغوجاراتية+Luqadda qer-qeesiya+النيبالية+Luqadda yuruuba+الليتوانية+الدرية+الصربية+الصومالية+Luqadda kiniya ruwadiga+الرومانية+المجرية+التشيكية+الموري+Luqadda malgaashka+Luqadda Oromaha+Luqadda kinaadiga+الولوف+Luqadda Asariga+الأوكرانية+الجورجية+المقدونية