«مَنْ سَأَلَ اللهَ الشَّهَادَةَ بِصِدْقٍ بَلَّغَهُ اللهُ مَنَازِلَ الشُّهَدَاءِ، وَإِنْ مَاتَ عَلَى فِرَاشِهِ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Sahli bin Hanif -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Atakayemuomba Mwenyezi Mungu shahada (yaani kufa shahidi) kwa ukweli, basi atamfikisha daraja ya mashahidi hata kama atafia juu ya godoro lake".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Katika hadithi kumebainishwa kuwa na nia ya kweli ni sababu ya kufikia malipo na thawabu, nakuwa atakayenuia jambo katika mambo mema basi atalipwa kwa hilo, hata kama hatoweza kulifanya, na miongoni mwa hilo ni yule atakayeomba apate shahada (afe vitani) katika njia ya Mwenyezi Mungu na kuinusuru dini yake kiukweli toka moyoni mwake, Mwenyezi Mungu atamuandikia malipo ya mashahidi hata kama hatofanya matendo yao na akafia sehemu nyingine isiyokuwa jihadi.