+ -

عَنِ ‌ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا قَالَ:
كَانَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَليهِ وَسَلَّمَ لا يَعْرِفُ فَصْلَ السُّورةِ حَتَّى تَنْزِلَ عَليْهِ {بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ}.

[صحيح] - [رواه أبو داود] - [سنن أبي داود: 788]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- amesema:
Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, hajui kitenganishi kati ya Sura na Sura nyingine mpaka imteremkie {Bismillahir Rahmanir Rahiim}.

[Sahihi] - [Imepokelewa na Abuu Daud] - [سنن أبي داود - 788]

Ufafanuzi

Anaweka wazi Bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- amesema: kuwa Sura za Qur'ani tukufu zilikuwa zikiteremka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- haikuwa ikijulikana kitenganishi chake wala mwisho wake mpaka imteremkie: {Bismillahir Rahmanir Rahiim} basi wakati huo ndipo hujua kuwa Sura iliyotangulia imekwisha, na hiyo Bismillahi ni mwanzo wa Sura mpya.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kimalayo Kitelguu Burmese Thai Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية Luqadda qer-qeesiya النيبالية Luqadda yuruuba الليتوانية الدرية الصربية الصومالية الطاجيكية Luqadda kiniya ruwadiga الرومانية التشيكية Luqadda malgaashka Kiitaliano Luqadda Oromaha Luqadda kinaadiga Luqadda Asariga الأوزبكية الأوكرانية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Bismillah hutumika kuzitenganisha Sura, isipokuwa kati ya Suratul Anfaal na Suratu t-taubah.
Ziada