+ -

عن ابن مسعود رضي الله عنه قال: ذُكِرَ عند النبي صلى الله عليه وسلم رجل نام ليلة حتى أصبح، قال: «ذاك رجل بال الشيطان في أُذُنَيْهِ - أو قال: في أُذُنِه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abdullahi bin Masoud -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema:
Alitajwa kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake mtu mmoja aliyelala usiku mpaka pakapambazuka, akasema: "Huyo ni mtu aliyekojolewa na Shetani ndani ya masikio yake, au alisema: ndani ya sikio lake".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح البخاري - 3270]

Ufafanuzi

Alitajwa kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake mtu mmoja aliyelala mpaka pakapambazuka na Jua likachomoza na wala hakunyanyuka kwenda katika swala ya faradhi, akasema rehema na amani ziwe juu yake: Huyo ni mtu ambaye Shetani kakojoa ndani ya sikio lake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kiassam الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ni karaha kuacha kusimama usiku, nakuwa hilo ni kwa sababu ya Shetani.
  2. Kutahadhari na Shetani anayemkalia mwanadam katika njia zote; ili amkinge na kuzuia kati yake na kumtii Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  3. Amesema bin Hajari: Kauli yake: "Hakusimama kuswali" Makusudio yake ni aina ya sala, na inawezekana kuwa ni ahadi, na inakusudiwa ni swala ya usiku au swala ya faradhi.
  4. Amesema Twaibi: Limetajwa sikio pekee, japokuwa jicho ndio linastahiki zaidi kulala ikiwa ni ishara ya uzito wa usingizi, kwa sababu masikio ndio nyenzo za umakini, na umetajwa mkojo; kwa sababu ndio mwepesi kupenya katika njia za sikio, na mwepesi kutembea katika mishipa, na kusababisha uvivu katika viungo vyote.