Aina:
+ -

عَنْ أَبِي بُرْدَةَ، عَنْ أَبِيهِ أَبِي مُوسَى الأَشْعَريِّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ:
أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ بَعَثَهُ إِلَى اليَمَنِ، فَسَأَلَهُ عَنْ أَشْرِبَةٍ تُصْنَعُ بِهَا، فَقَالَ: وَمَا هِيَ؟، قَالَ: «البِتْعُ وَالمِزْرُ»، فَقِيلَ لِأَبِي بُرْدَةَ: مَا البِتْعُ؟ قَالَ: نَبِيذُ العَسَلِ، وَالمِزْرُ: نَبِيذُ الشَّعِيرِ، فَقَالَ: «كُلُّ مُسْكِرٍ حَرَامٌ» خرجه البخاري. وَخَرَّجَهُ مُسْلِمٌ وَلَفْظُهُ: قَالَ: بَعَثَنِي رَسُولُ اَلله أَنَا وَمُعَاذٌ إِلَى اَليَمَنِ، فَقُلْتُ: يَا رَسُولُ اَللَّهِ! إِنَّ شَرَابًا يُصْنَعُ بِأَرْضِنَا يُقَال لَهُ: المِزَرُ مِنَ الشَّعِيرِ، وَشَرَابٌ يُقَالُ لَهُ: البِتْعُ مِنَ العَسَلِ، فَقَالَ: «كُلُّ مُسْكِرٍ حَرَامٌ». وَفِي رِوَايَةٍ لِمُسْلِمٍ: «فَقَالَ: كُلُّ مَا أَسْكَرَ عَنِ الصَّلَاةِ فَهُوَ حَرَامٌ». وَفِي رِوَايَةٍ لَهُ: «وَكَانَ رَسُولُ الله قَدْ أُعْطِيَ جَوَامِعَ الكَلِمِ بِخَوَاتِمِهِ، فَقَالَ: أَنْهَى عَنْ كُلِّ مُسْكِرٍ أَسْكَرَ عَنْ الصَّلَاةِ».

[صحيح] - [رواه البخاري ومسلم] - [الأربعون النووية: 46]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Buraida, kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abuu Musa A-Ash'ari radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake:
Ya kwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake alimtuma kwenda Yemen, akamuuliza kuhusu vinywaji fulani vinavyotengenezwa huko, akasema: Ni vipi hivyo?, akasema: "Ni Bit'u na Mizru" akaulizwa Abuu Buraida: Bit'u ni nini? Akasema: Ni mvinyo wa Asali, na Mizru: Ni mvinyo wa ngano, akasema: "Kila kilevi ni haramu" Ameitoa Bukhari.

-

Ufafanuzi

Anaeleza Abuu Musa Al-Ash'ari radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake ya kwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake alimtuma kwenda Yemen, akamuuliza kuhusu vinywaji vinavyo tengenezwa huko je ni haramu, akamuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu hilo. Akasema Abuu Musa radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: Ni Bit'u: Yaani mvinyo wa Asali, na Muruuz: Ni mvinyo wa ngano. Akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake na alikuwa amepewa maneno machache yenye maana pana: "Kile chenye lewesha ni haramu".

Katika Faida za Hadithi

  1. Mvinyo: Ni maji yanayotiwa tende ndani yake au Asali au Ngano na mfano wake; yakafyonza ladha na utamu, na wakati mwingine huenda yakapata kilevi baada ya hapo yakawa ni kilevi.
  2. Hadithi hii ni kanuni katika kuharamisha aina zote za vilevi kama pombe na bangi na nyinginezo.
  3. Umuhimu wa kuuliza yale anayoyahitajia Muislamu.
  4. Ilikuwa mwanzo ilipoharamishwa pombe ni wakati swala inapoingia, pindi waliposwali baadhi ya watu waliohamia Madina na wakasoma wakachanganya ndani ya kisomo chao; ikateremka kauli yake: "Enyi mlio amini! Msiikaribia swala hali nyinyi mmelewa mpaka mjue mnachokisema" [An Nisaa: 43]. Na alikuwa muadhini wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akinadi: Msiikaribie swala hali yakuwa mmelewa. Kisha Mwenyezi Mungu akaiharamisha moja kwa moja kwa kauli yake: "Enyi mlio amini! Bila ya shaka ulevi na kamari, na kuabudu masanamu, na kupiga ramli ni uchafu katika kazi ya Shetani. Basi jiepusheni navyo, ili mpate kufanikiwa (90) Hakika Shetani anataka kutia kati yenu uadui na chuki kupitia ulevi na kamari, na akuzuieni kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kusali. Basi je, mmeacha?" [Al-Maidah: 90,91].
  5. Nikuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu aliiharamisha pombe kulingana na madhara na maovu makubwa yaliyomo.
  6. Kinachozingatiwa katika uharamu ni uwepo wa sifa ya kilevi; mvinyo ukisifika kwa sifa ya kilevi basi ni haramu, na usipokuwa na kilevi basi ni halali.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Kibangali Kituruki Lugha ya Kirashia Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Thai Pashto Kiassam Albanian الأمهرية الغوجاراتية Luqadda qer-qeesiya النيبالية الدرية الصربية الطاجيكية Luqadda kiniya ruwadiga المجرية التشيكية الموري الولوف Luqadda Asariga الأوزبكية الأوكرانية الجورجية المقدونية الخميرية
Kuonyesha Tarjama
Aina tofauti
Ziada