Aina:
+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ صَخْرٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم يَقُولُ:
«مَا نَهَيْتُكُمْ عَنْهُ فَاجْتَنِبُوهُ، وَمَا أَمَرْتُكُمْ بِهِ فَافْعَلُوا مِنْهُ مَا اسْتَطَعْتُمْ، فَإِنَّمَا أَهْلَكَ الَّذِينَ مِنْ قَبْلِكُمْ كَثْرَةُ مَسَائِلِهِمْ، وَاخْتِلَافُهُمْ عَلَى أَنْبِيَائِهِمْ».

[صحيح] - [رواه البخاري ومسلم] - [الأربعون النووية: 9]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira Abdul-Rahman bin Swakhar -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Nilimsikia Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- akisema:
"Yale niliyokukatazeni basi yaepukeni, na yale niliyokuamrisheni basi fanyeni katika hayo kadiri muwezavyo, na hakika waliangamia wale waliokuwa kabla yenu, kwa kukithiri maswali yao, na kuhitilafiana kwao na Manabii wao".

-

Ufafanuzi

Ametubainishia sisi Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kuwa atakapotukataza kitu basi ni wajibu juu yetu kukiacha pasina kubagua, na atakapotuamrisha kwa chochote basi ni juu yetu kukifanya kile tunachokiweza. Kisha akatutahadharisha ili tusije kuwa kama baadhi ya umma zilizopita pindi walipokithirisha maswali juu ya Manabii wao ikiwa ni pamoja na kwenda kinyume nao, basi Mwenyezi Mungu akawaadhibu kwa aina mbali mbali za maangamivu na uharibifu, tunatakiwa tusiwe mfano wao ili tusiangamie kama walivyoangamia.

Katika Faida za Hadithi

  1. Hadithi ni kanuni katika kubainisha kuwa la wajibu ni kutekeleza amri na kujiepusha na makatazo.
  2. Katazo halikuruhusu kufanya chochote katika hayo, lakini amri imewekwa sharti la uwezo; kwa sababu kuacha ni jambo liko ndani ya uwezo na kufanya kunahitaji uwezo wa kuleta kitendo kilichoamrishwa.
  3. Makatazo yanakusanya kidogo na mengi; kwa sababu haiwezekani kuyaepuka ila kwa kuyaepuka kidogo yake na mengi yake, kwa mfano: Ametukataza riba hii inakusanya ndogo yake na kubwa yake.
  4. Kuacha sababu zinazopelekea katika haramu; kwa sababu hilo ni miongoni mwa maana za kuepeuka.
  5. Haitakiwi kwa mtu atakaposikia amri ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake aseme: Je ni wajibu au ni sunna?, bali anawajibika kwenda mbio kutekeleza; kwa kauli yake: "Yafanyeni katika hayo kadiri muwezavyo".
  6. Wingi wa maswali ni sababu ya kuangamia hasa hasa katika mambo ambayo haiwezekani kuyafikia, mfano kama mambo ya ghaibu, na namna ya hali ya siku ya Kiyama, usizidishe maswali ndani yake utaangamia, na ukawa ni king'ang'anizi na mtafuta mambo kwa undani.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Kibangali Kituruki Lugha ya Kirashia Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Thai Pashto Kiassam Albanian الأمهرية الغوجاراتية Luqadda qer-qeesiya النيبالية الدرية الصربية الطاجيكية Luqadda kiniya ruwadiga المجرية التشيكية الموري Luqadda kinaadiga الولوف Luqadda Asariga الأوزبكية الأوكرانية الجورجية المقدونية الخميرية
Kuonyesha Tarjama
Aina tofauti
Ziada