عن أبي رقية تميم بن أوس الداري رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «الدين النصيحة» قلنا: لمن؟ قال: «لله، ولكتابه، ولرسوله، ولأئمة المسلمين وعامتهم».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abii Ruqayya Tamiim bin Awsi Ad-daariy -Radhi za Allah zimuendee- kwamba Mtume -Rehma na amani za Allah zimwendee- amesema : " Dini ni nasaha" tukasema : Ni kwa nani ?akasema: Kwa ajili ya Allah, na kwa ajili ya kitabu chake,na kwa ajili ya Mtume wake,na kwa ajili ya viongozi wa Kiislamu na waislamu kwa ujumla".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Imekuja dini hii tukufu na mafundisho ya kufikisha nasaha kwa Ikhlas,na kutufunza tuamini na tukubali upweke wa Allah alie takasika na kutukuka,na tumtakase na kila mapungufu,na tumsifu kwa sifa za ukamilifu,nakwamba Qur-ani tukufu ni maneno yake ambayo kayateremsha wala sio kiumbe,tunazifanyia kazi hukmu zake,na tunayaamini yaliyo na utata ndani yake,na tunamsadikisha Mtume-Rehma na amani zimwendee-kwa yale aliyokuja nayo,na tunatekeleza amri zake na kuepuka makatazo yake,na tunawapa nasaha viongozi wa Kiislamu kwa kuwaunga mkono katika haki,na kuwaongoza katika yale wasiyo yajua,na kuwakumbusha pale walipo sahau au kughafilika,na tunawaongoza waislamu kwa ujumla kunako haki,na tunazuia shari zetu kwao na hata kutoka kwa wengine kwa kadiri ya uwezo wetu,na tunawaamrisha mema na kuwakataza mabaya, na ujumla wa nasaha zetu kwao ni kwamba: Tunawapendelea yale ambayo kila mmoja wetu anayapendelea katika nafsi yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Amri ya kutoa nasaha.
  2. Ukubwa wa nafasi ya nasaha katika dini, ndio maana ikaitwa dini.
  3. Nikuwa dini inakusanya maneno na matendo.
  4. Kwa mwanachuoni aegemee zaidi katika uelewa wa yale anayoyafikisha kwa msikilizaji, na wala asimzidishie katika ufafanuzi mpaka muulizaji amuulize mwenyewe, ili nafsi yake ipate shauku kwake wakati huo, yanakita zaidi ndani ya nafsi yake kuliko ambavyo angemueleza moja kwa moja.
  5. Uzuri wa mafundisho ya Mtume rehema na Amani ziwe juu yake kiasi ambacho anataja kitu kwa ujumla kisha anakifafanua.
  6. Pupa ya maswahaba Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao juu ya elimu nakuwa wao hawakuacha kitu ambacho wanahitaji ufafanuzi wake ispokuwa walikiuliza.
  7. Kuanza na jambo la muhimu zaidi kisha linalofuata,kiasi ambacho ameanza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kwa nasaha kwaajili ya Mwenyezi Mungu, kisha kitabu chake, kisha kwa Mtume rehema na Amani ziwe juu yake- kisha kwa viongozi wa waislamu, kisha watu wote.
  8. Kutilia mkazo maneno kwa kuyarudia kwaajili ya kuyazingatia na kufanya yafahamike, kama ilivyokuja katika riwaya ya imamu Ahmadi: "Dini ni nasaha" Mara tatu.
  9. Nasaha ni kwa wote.