عن أبي رقية تميم بن أوس الداري رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «الدين النصيحة» قلنا: لمن؟ قال: «لله، ولكتابه، ولرسوله، ولأئمة المسلمين وعامتهم».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abii Ruqayya Tamiim bin Awsi Ad-daariy -Radhi za Allah zimuendee- kwamba Mtume -Rehma na amani za Allah zimwendee- amesema : " Dini ni nasaha" tukasema : Ni kwa nani ?akasema: Kwa ajili ya Allah, na kwa ajili ya kitabu chake,na kwa ajili ya Mtume wake,na kwa ajili ya viongozi wa Kiislamu na waislamu kwa ujumla".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Imekuja dini hii tukufu na mafundisho ya kufikisha nasaha kwa Ikhlas,na kutufunza tuamini na tukubali upweke wa Allah alie takasika na kutukuka,na tumtakase na kila mapungufu,na tumsifu kwa sifa za ukamilifu,nakwamba Qur-ani tukufu ni maneno yake ambayo kayateremsha wala sio kiumbe,tunazifanyia kazi hukmu zake,na tunayaamini yaliyo na utata ndani yake,na tunamsadikisha Mtume-Rehma na amani zimwendee-kwa yale aliyokuja nayo,na tunatekeleza amri zake na kuepuka makatazo yake,na tunawapa nasaha viongozi wa Kiislamu kwa kuwaunga mkono katika haki,na kuwaongoza katika yale wasiyo yajua,na kuwakumbusha pale walipo sahau au kughafilika,na tunawaongoza waislamu kwa ujumla kunako haki,na tunazuia shari zetu kwao na hata kutoka kwa wengine kwa kadiri ya uwezo wetu,na tunawaamrisha mema na kuwakataza mabaya, na ujumla wa nasaha zetu kwao ni kwamba: Tunawapendelea yale ambayo kila mmoja wetu anayapendelea katika nafsi yake.