عَنِ ابْنِ مَسْعُودٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:

«لَقِيتُ إِبْرَاهِيمَ لَيْلَةَ أُسْرِيَ بِي فَقَالَ: يَا مُحَمَّدُ، أَقْرِئْ أُمَّتَكَ مِنِّي السَّلاَمَ، وَأَخْبِرْهُمْ أَنَّ الجَنَّةَ طَيِّبَةُ التُّرْبَةِ عَذْبَةُ الْمَاءِ، وَأَنَّهَا قِيعَانٌ، وَأَنَّ غِرَاسَهَا سُبْحَانَ اللهِ وَالحَمْدُ لِلَّهِ وَلاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَاللَّهُ أَكْبَرُ».
[حسن بشواهده] - [رواه الترمذي]
المزيــد ...

Kutoka kwa bin Mas'udi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Nilikutana na Ibrahimu usiku niliochukuliwa, Akasema: Ewe Muhammadi wafikishie umma wako salamu zangu, na uwaeleze kuwa pepo ina udongo mzuri, ina maji matam, nakuwa imenyooka na kulingana sawa, nakuwa mimea yake: ni (kusema) Sub-haana llaah -Ametakasika Mwenyezi Mungu, Na Alhamdulillaah -Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu, Na Laa ilaaha illa llaah -Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na Allaahu Akbar -Mwenyezi Mungu Mkubwa".
Ni nzuri - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Anaeleza Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa yeye alikutana na Ibrahim Amani iwe juu yake- usiku aliopandishwa mbinguni, nakuwa yeye alimueleza kuwa afikishe na awasilishe salamu kwa umma wake -Rehema na Amani ziwe juu yake- Na awaeleze kuwa pepo ina udongo mzuri, na imekuja katika hadithi nyingine kuwa udongo wake ni za'farani, kama ilivyokuja katika riwaya ya Tirmidhiy pale walipomuuliza maswahaba -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuhusu pepo akasema: "Na udongo wake ni Za'farani" na kwa Imamu Ahmad "Na udongo wake ni mwekundu na ni wa za'faran". "Ina maji matam" Yaani nikuwa maji yake ni matam na yanaladha tam, kama alivyosema Mtukufu-: (kuna Mito ya maji yasiyovunda) [Muhammad: 15] Yaani hayaharibiki kwa chumvi kuchacha au kinginecho, ikiwa kama pepo ina udongo mzuri na maji matam, basi mimea yake bila shaka itakuwa mizuri mno, na kuipanda kwake kunapatikana kwa maneno, nayo ndiyo mema yenye kubakia. "Nayo ni tambarare" Nayo ni sehemu pana iliyolingana katika ardhi. "Nakuwa mimea yake" Yaani vinavyopandwa katika sehemu hiyo pana ni, "Sub-haana llaah, na Alhamdulillaah, na Laa ilaaha illa llaah, na Allaahu Akbar" Na maana yake: Nikuwa mimea yake ni maneno mazuri: Tasbihi (kusema sub-haana llaah) Tahmid (kusema Alhamdulillaah), Na Tahliil (kusema: Laa ilaaha illa llaah), hivyo kila mwenye kumtukuza Mwenyezi Mungu na akampwekesha basi anapandiwa mti wa mtende peponi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama

Maana ya Maneno

الملاحظة
قيعان: هو المكان الواسع المستوي من الأرض، يعلوه ماء السماء، فيمسكه ويستوي نباته.
المكان الواسع
النص المقترح هو المكان الواسع المستوي من الأرض، يعلوه ماء السماء، فيمسكه ويستوي نباته.