كُنَّا مَعَ رَسُولِ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، إِذْ سَمِعَ وَجْبَةً، فَقَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «تَدْرُونَ مَا هَذَا؟» قَالَ: قُلْنَا: اللهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ، قَالَ: «هَذَا حَجَرٌ رُمِيَ بِهِ فِي النَّارِ مُنْذُ سَبْعِينَ خَرِيفًا، فَهُوَ يَهْوِي فِي النَّارِ الْآنَ حَتَّى انْتَهَى إِلَى قَعْرِهَا».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Tulikuwa pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ghafla akasikia kishindo, akasema: "Hivi mnajua ni nini hicho?" tukasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndiyo wajuzi. Akasema: "Hilo ni jiwe lililotupwa motoni tangu miaka sabini, anaporomoka motoni sasa hivi mpaka kaishia katika kina chake ndio maana mkasikia kishindo chake".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Walikuwa maswahaba pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- wakasikia kishindo, akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- je mnajua ni nini hiki? wakasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndio wajuzi. Akasema: Hii ni sauti ya jiwe limetupwa motoni tangu miaka sabini, ndio linateremka motoni sasa hivi lilipofika katika shimo lake mkasikia taharuki ya moto kwasababu ya jiwe kushuka ndani yake.