Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Fanyeni haraka kufanya matendo kuna fitina nzito kama kipande cha usiku wa giza, anaamka mtu akiwa muislamu anafika jioni akiwa kafiri, na anashinda akiwa muumini anaamka asubuhi akiwa kafiri, anauza dini yake kwa thamani ndogo ya dunia"
الملاحظة
عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم : «بَادِرُوا بالأعمال فِتَنًا كَقِطَعِ الليل المُظْلِمِ، يُصْبِحُ الرجلُ مؤمنا ويُمْسِي كافرا، ويُمْسِي مؤمنا ويُصْبِحُ كافرا، يبيعُ دينه بِعَرَضٍ من الدنيا».
https://hadeethenc.com/ur/browse/hadith/3138
النص المقترح عربي
الملاحظة
لماذا لا يذكر الموقع الإلكتروني رقم الحديث واسم راوي الحديث في قسم الحديث؟
النص المقترح عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم : «بَادِرُوا بالأعمال فِتَنًا كَقِطَعِ الليل المُظْلِمِ، يُصْبِحُ الرجلُ مؤمنا ويُمْسِي كافرا، ويُمْسِي مؤمنا ويُصْبِحُ كافرا، يبيعُ دينه بِعَرَضٍ من الدنيا».
الملاحظة
هذا الحديث ضعيف لا أصل له، باطل لا كلام النبي ، اتقوا الله لا تنشروا الكذب على الرسول ولا تضلوا الناس
بَادِرُوا بِالأَعْمَالِ فِتَنا كَقِطَعِ اللَّيْلِ الْمُظْلِمِ. يُصْبِحُ الرَّجُلُ فِيْهَا مُؤْمِناً وَيُمْسِي كَافِراً. أَوْ يُمْسِي مُؤْمِناً وَيُصْبِحُ كَافِراً. يَبِيعُ دِينَهُ بِعَرَضٍ مِنَ الدُّنْيَا
النص المقترح لا يوجد...
[Sahihi] - [Imepokelewa Imamu Muslim] - [Swahiih Muslim - 118]Ufafanuzi
Mtume rehema na amani ziwe juu yake anamtaka Muumini kufanya hima na kufanya mambo mengi ya kheri kabla hayajashindikana, na akashughulishwa na kuja kwa fitna na mambo yenye kutatiza yanayoweza kuzuia kufanya matendo mema, na kuyaziba, na hali ni kwamba, ni giza kama kipande cha usiku ambao ndani yake haki imechanganyika na batili, na kukawawia vigumu watu kutofautisha baina yake, na kwa sababu ya ukali wake (Fitina hiyo), mtu huchanganyikiwa kiasi cha kuamka muumini, na kufika jioni ni kafiri, kushinda Muumini na kufika asubuhi kawa kafiri, anaiacha dini yake kwa starehe za muda mfupi za dunia.
Katika Faida za Hadithi
Ni lazima kushikamana na dini, na kwenda mbio katika matendo mema kabla ya vikwazo kuzuia hilo.
Hii ni ishara ya mfuatano wa majaribu yenye kupoteza katika zama za mwisho, na kwamba wakati wowote fitina moja inapotoweka, fitina ingine linafuata.
Ikiwa dini ya mtu ni dhaifu na akaiacha kwa kubadilishana na mambo ya kidunia, kama vile pesa au vitu vingine, hii ni sababu ya kupotoka kwake, kuacha dini, na kuingia kwake kwenye vishawishi na fitina.
Kuna ushahidi katika Hadithi kwamba matendo mema ni njia ya kuokoka na fitina.
Kuna aina mbili za fitina: Fitina ya shubuha (Mambo yenye utata), na tiba yake ni elimu, na fitina ya matamanio, na tiba yake ni imani na subira.
Hadithi inaashiria kuwa mwenye matendo kidogo, fitina kwake ni nyepesi zaidi, na mwenye matendo mengi anatakiwa asihadaike na alichonacho, bali aongeze zaidi.
Lugha:Lugha ya kiingerezaLugha ya KiurduKiispaniaLugha ya KiindonesiaKibangaliLugha ya kifaransaKiturukiLugha ya KirashiaLugha ya KibosniaKisin-halaKihindiKichinaKifursiKivetenamuKitagalogiKikurdiKihausaKirenoKimalayoKitelguuKunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiriThaiGermanPashtoKiassamAlbanianالسويديةالأمهريةالهولنديةالغوجاراتيةLuqadda qer-qeesiyaالنيباليةLuqadda yuruubaالليتوانيةالدريةالصربيةالصوماليةLuqadda kiniya ruwadigaالرومانيةالمجريةالتشيكيةالموريLuqadda malgaashkaLuqadda OromahaLuqadda kinaadigaالولوفLuqadda AsarigaالأوزبكيةالأوكرانيةالجورجيةالمقدونيةالخميريةالبنجابيةالماراثيةZiada (54)