عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ بُسْرٍ رَضِيَ اللَّهِ عَنْهُ قَالَ: أَتَى النَّبِيَّ رَجُلٌ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّهِ! إِنَّ شَرَائِعَ الإِسْلَامِ قَدْ كَثُرَتْ عَلَيْنَا، فَبَابٌ نَتَمَسَّكُ بِهِ جَامِعٌ؟ قَالَ:
«لاَ يَزَالُ لِسَانُكَ رَطْبًا مِنْ ذِكْرِ اللَّهِ».
وفي رواية: مِنْ حَدِيثِ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ: آخِرُ مَا فَارَقْتُ عَلَيْهِ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنْ قُلْتُ: أَيُّ الأَعْمَالِ خَيْرٌ وَأَقْرَبُ إِلَى اللَّهِ؟ قَالَ: «أَنْ تَمُوتَ وَلِسَانُكَ رَطْبٌ مِنْ ذِكْرِ اللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ».
[صحيح] - [رواه أحمد والترمذي وابن ماجه وابن حبان] - [الأربعون النووية: 50]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdallah bin Busri radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amesema: Mtu mmoja alikuja kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Hakika sheria za Uislamu zimekuwa nyingi kwetu, ni mlango gani tushikamane nao uliokusanya mambo mengi? Akasema:
"Ulimi wako usiache kuwa mbichi kwa kumtaja Mwenyezi Mungu". Na katika riwaya nyingine: Miongoni mwa hadithi za Muadhi radhi za Mwneyezi Mungu ziwe juu yake: Maneno ya mwisho niliochana na Mtume rehema na amani ziwe juu yake nilisema: Ni amali ipi bora na iko karibu zaidi na Mwenyezi Mungu? Akasema: "Ni ufe hali yakuwa ulimi wako ni mbichi kwa kumtaja Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na Kutukuka".
[Sahihi] - [Imepokelewa na Ahmad, Tirmidhiy, Ibn Majah na Ibn Hibban] - [Al-Arbauna An-Nawawiyah - 50]
Mtu mmoja alilalamika kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa ibada za sunna zimekuwa nyingi kwake mpaka zikamshinda kwa sababu ya udhaifu wake, kisha akamuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake amuelekeze katika amali nyepesi itakayompa thawabu nyingi atakayoshikamana nayo na adumu nayo.
Mtume rehema na amani ziwe juu yake akamuelekeza kuwa ulimi wake uwe mbichi utikisike kwa kudumu kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu kila wakati na kila hali; kama kumsabihi na kumhimidi na kumtaka msamaha na kumuomba na mfano wake.