Aina:

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ سَعْدِ بْنِ مَالِكِ بْنِ سِنَانٍ الخُدْرِيّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«لَا ضَرَرَ وَلَا ضِرَارَ».

[حسن] - [رواه ابن ماجه، والدارقطني، وغيرهما مسندًا] - [الأربعون النووية: 32]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Saidi Sa'di bin Maaliki bin SInani Al-Khudry -radhi za Allah ziwe juu yake- yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Haifai kujidhuru wala kumdhuru mwingine."

[Ni nzuri (Hasan)] - [Imepokelewa na Ibnu Maajah, Daaruqutni na wengineo huku inafika kwa Mtume] - [Al-Arbauna An-Nawawiyah - 32]

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- kuwa ni lazima kuzuia madhara kwa aina zake zote na sababu zake zote kwako na kwa wengine, ni haramu kwa yeyote kujiudhi mwenyewe na mwingine kwa kiwango sawa. Na ni haramu kwake kukabiliana na madhara kwa madhara; kwa sababu madhara hayaondoshwi kwa madhara, isipokuwa kama itakua katika njia ya kulipiza kisasi pasina kuvuka mipaka.

Katika Faida za Hadithi

  1. Katazo la kulipiza kwa zaidi ya vile ulivyofanyiwa.
  2. Mwenyezi Mungu hakuwaamrisha waja wake lolote lenye kuwadhuru.
  3. Hadithi ni kanuni katika kuharamisha kujidhuru, na kudhuru kwa kauli au vitendo au kuacha.
  4. Katika kanuni za sheria: Ni "Madhara huondoshwa", Hivyo, sheria haikubaliani na madhara, na inakataza kujidhuru.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (53)
Aina tofauti
Ziada