عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:

«خَيْرُ يَوْمٍ طَلَعَتْ عَلَيْهِ الشَّمْسُ يَوْمُ الْجُمُعَةِ، فِيهِ خُلِقَ آدَمُ، وَفِيهِ أُدْخِلَ الْجَنَّةَ، وَفِيهِ أُخْرِجَ مِنْهَا، وَلَا تَقُومُ السَّاعَةُ إِلَّا فِي يَوْمِ الْجُمُعَةِ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Siku bora lililochomoza jua ndani yake ni siku ya ijumaa: Ndani yake kaumbwa Adam, na ndani yake kaingizwa peponi, na ndani yake katolewa humo".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-: Kuwa siku bora ambayo limechomoza ndani yake ni siku ya ijumaa, ndani yake kaumbwa Adam, naye ndiye baba wa watu, alimuumba Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa mkono wake, alimuumba kwa udongo na siku hiyo ilikua ni siku ya ijumaa, na ndani yake aliingizwa pepo ya mafikio (Jannatul Ma' awaa) ambayo watafikia watu, alimuingiza Mwenyezi Mungu peponi yeye na mke wake, na katika siku ya ijumaa alimuamrisha Mwenyezi Mungu -Mtukufu- kutoka ndani yake, na haikuwa kutolewa kwake ni kwasababu ya kudhalilishwa, bali ni kwasababu ya hekima na malengo ya Mwenyezi Mungu Mtukufu yalipelekea hivyo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno Thai Kiassam الدرية
Kuonyesha Tarjama

Maana ya Maneno