عَنْ أَبِي بَكْرٍ الصِّدِّيقِ رضي الله عنه أَنَّهُ قَالَ: أَيُّهَا النَّاسُ، إِنَّكُمْ تَقْرَؤُونَ هَذِهِ الآيَةَ: {يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَيْكُمْ أَنْفُسَكُمْ لاَ يَضُرُّكُمْ مَنْ ضَلَّ إِذَا اهْتَدَيْتُمْ}، وَإِنِّي سَمِعْتُ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ:

«إِنَّ النَّاسَ إِذَا رَأَوْا الظَّالِمَ فَلَمْ يَأْخُذُوا عَلَى يَدَيْهِ أَوْشَكَ أَنْ يَعُمَّهُمُ اللَّهُ بِعِقَابٍ مِنْهُ».
[صحيح] - [رواه أبو داود والترمذي والنسائي في الكبرى وابن ماجه وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuubakari As swiddiq -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Enyi watu, hakika nyinyi mnaisoma aya hii: (Enyi mlioamini zirekebisheni nafsi zenu hatokudhuruni atakayepotea mtakapoongoka) [Al-Maaidah:105], Na hakika mimi nilimsikia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- Akisema: "Hakika watu watakapomuona mtu dhalimu (muovu) na wakawa hawakumzuia wako karibu mno Mwenyezi Mungu kuwafunika wote kwa adhabu itokayo kwake".
Sahihi - Imepokelewa na Ibnu Maajah

Ufafanuzi

Alisema Abuubakari As swiddiq -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Enyi watu, hakika nyinyi mnaisoma aya hii (Enyi mlioamini zirekebisheni nafsi zenu hatokudhuruni atakayepotea mtakapoongoka) [Al-Maaidah:105], na mnaielewa kuwa mtu atakapoongoka mwenyewe binafsi basi hautomdhuru upotofu wa watu; kwasababu yeye binafsi kanyooka, atakaponyooka mwenyewe binafsi basi mambo ya watu wengine yako juu ya Mwenyezi Mungu aliyetakasika na kutukuka, na maana hii ni maana mbovu, kwasababu Mwenyezi Mungu kaweka sharti kuwa ili aliyepotea asitudhuru, ni sisi tuongoke, akasema: (Hatokudhuruni atakayepotea mtakapoongoka), na katika sehemu ya kuongoka: ni sisi tuamrishe mema na tukataze mabaya, ikiwa hili ni katika kuongoka, basi ni lazima ili tusalimike na madhara kwa kuamrisha mema na kukataza mabaya, na kwaajili hii alisema -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: na mimi nilimsikia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akisema: "Hakika watu watakapouona uovu na wakawa hawakuukemea, au hawakumzuia muovu, inahofiwa kuwa Mwenyezi Mungu atawafunika wafunika wote kwa adhabu itokayo kwake" Yaani maana yake nikuwa wao watadhuriwa na wale waliopotea watakapokuwa wanamuona aliyepotea na wala hawamuamrishi mema, wala hawamkatazi maovu, basi hapo wanakaribia zaidi Mwenyezi Mungu kuwafunika wote kwa adhabu; mfanyaji na aliyejisahau, mfanyaji wa maovu, na aliyejisahau ambaye hakuukemea uovu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Thai Kiassam الدرية
Kuonyesha Tarjama

Maana ya Maneno