+ -

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنَّهُ قَالَ:
«لَا يَمْنَعَنَّ رَجُلًا مِنْكُمْ مَخَافَةُ النَّاسِ أَنْ يَتَكَلَّمَ بِالْحَقِّ إِذَا رَآهُ أَوْ عَلِمَهُ».

[صحيح] - [رواه الترمذي وابن ماجه وأحمد] - [مسند أحمد: 11403]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abii Saidi Al-Khudry radhi za Allah ziwe juu yake kutoka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake amesema:
"Kusimzuie mmoja wenu kuwaogopa watu akaache kusema haki atakapoiona au kuijua".

[Sahihi] - - [مسند أحمد - 11403]

Ufafanuzi

Alihutubia Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa Maswahaba zake, na miongoni mwa mambo aliyowausia ni kuwa Muislamu isimzuie hofu na kuowaogopa watu na nguvu yao akaacha kusema haki au kuiamrisha atakapoiona au kuijua.

Katika Faida za Hadithi

  1. Himizo la kuidhihirisha haki na kutoificha kwa kuwaogopa watu.
  2. Kusema haki haimaanishi ni kutokuwa na adabu katika mfumo wa kauli zake na hekima na mawaidha mazuri ndani yake.
  3. Uwajibu wa kuondoa uovu, na kutanguliza haki ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuliko masilahi ya watu yanayopingana na hilo.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiindonesia Kisin-hala Kivetenamu Kihausa Kiassam الهولندية الغوجاراتية الرومانية المجرية الجورجية
Kuonyesha Tarjama