«إِنَّمَا مَثَلُ الْجَلِيسِ الصَّالِحِ وَالْجَلِيسِ السَّوْءِ كَحَامِلِ الْمِسْكِ وَنَافِخِ الْكِيرِ، فَحَامِلُ الْمِسْكِ: إِمَّا أَنْ يُحْذِيَكَ، وَإِمَّا أَنْ تَبْتَاعَ مِنْهُ، وَإِمَّا أَنْ تَجِدَ مِنْهُ رِيحًا طَيِّبَةً، وَنَافِخُ الْكِيرِ: إِمَّا أَنْ يُحْرِقَ ثِيَابَكَ، وَإِمَّا أَنْ تَجِدَ رِيحًا خَبِيثَةً».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Musa Al-Ash'ariy- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika bila shaka mfano wa rafiki mwema na rafiki muovu, ni kama mfano wa mbeba miski, na mfua vyuma, mbeba miski: ima akupe, na ima ununue toka kwake, na ima unaweza kupata toka kwake harufu nzuri, Na mfua vyuma: Ima achome nguo zako, na ima upate toka kwake harufu mbaya".
Amehimiza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithi hii juu ya umuhimu wa kuchagua urafiki mzuri, Na akaeleza -ziwe juu yake sala na salamu- kuwa mfano wa rafiki mzuri ni kama mbeba miski: Ima akupe bure, na ima ununue toka kwake, na ima upate toka kwake harufu nzuri, Ama rafiki muovu -Mwenyezi Mungu atuepushe- yeye ni kama mfua vyuma: Ima aunguze nguo zako kwa yale yanayokurukia katika cheche, na ima upate toka kwake harufu mbaya.