+ -

عَنْ عَائِشَةَ أُمِّ المُؤْمِنينَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ:
مَا أَكَلَ آلُ مُحَمَّدٍ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَكْلَتَيْنِ فِي يَوْمٍ إِلَّا إِحْدَاهُمَا تَمْرٌ.

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 6455]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Aisha mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake amesema:
Hakuwahi kula Muhammadi rehema na amani ziwe juu yake milo miwili kwa siku isipokuwa mlo mmoja utakuwa ni tende.

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح البخاري - 6455]

Ufafanuzi

Anaeleza mama wa waumini Aisha radhi za Allah ziwe juu yake kwamba watu wa nyumba ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake hawakuwahi kula milo miwili kwa siku moja isipokuwa mlo mmoja kati ya hiyo utakuwa ni tende.

Katika Faida za Hadithi

  1. Unyenyekevu wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake na watu wa nyumba yake, huenda kuna wakati hawakupata mlo zaidi ya mmoja.
  2. Tende ilikuwa rahisi kwao kuliko chochote.
  3. Ubora wa kuipa nyongo dunia na kutosheka na kichache katika maisha, na kuwa hilo ni katika tabia za Mtume rehema na amani ziwe juu yake bwana wa Mitume.
  4. Kula milo miwili kwa siku ni katika mambo halali na yanayofaa, nayo ni katika desturi za Waarabu inafahamika, walikuwa wakila kwa siku milo miwili, chakula cha mchana, na chakula cha usiku.
Tafsiri: Lugha ya Kiindonesia Kibangali Kivetenamu Kikurdi Kireno Thai Kiassam الهولندية الدرية المجرية الجورجية المقدونية
Kuonyesha Tarjama