عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«اللهُمَّ إِنَّمَا أَنَا بَشَرٌ، فَأَيُّمَا رَجُلٍ مِنَ المُسْلِمِينَ سَبَبْتُهُ أَوْ لَعَنْتُهُ أَوْ جَلَدْتُهُ فَاجْعَلْهَا لَهُ زَكَاةً وَرَحْمَةً».
[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 2601]
المزيــد ...
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake:
"Ewe Mola wangu, hakika mimi ni mwanadamu, basi yeyote katika Waislamu niliyemtukana au kumlaani au kumpiga kwa mjeledi, basi hilo lifanye kwake kuwa ni utakaso na huruma".
[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 2601]
Aliomba Mtume rehema na amani ziwe juu yake akasema: Ewe Mola wangu, hakika mimi ni mwanadamu, hivyo basi, muumini yeyote niliyemuudhi au kumtukana au kumshutumu, au kumlaani, na nikamuombea kufukuzwa katika rehema yako, au nilimpiga mjeledi au kipigo chochote, basi lifanye hilo kwake kuwa ni utakaso na ibada na twahara na kafara na rehema utakayomhurumia kwayo.