عَنْ عَائِشَةَ أُمِّ المُؤْمِنينَ رَضِيَ اللهُ عَنْها قَالَتْ:
كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ إِذَا أَمَرَهُمْ أَمَرَهُمْ مِنَ الأَعْمَالِ بِمَا يُطِيقُونَ، قَالُوا: إِنَّا لَسْنَا كَهَيْئَتِكَ يَا رَسُولَ اللَّهِ، إِنَّ اللَّهَ قَدْ غَفَرَ لَكَ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِكَ وَمَا تَأَخَّرَ، فَيَغْضَبُ حَتَّى يُعْرَفَ الغَضَبُ فِي وَجْهِهِ، ثُمَّ يَقُولُ: «إِنَّ أَتْقَاكُمْ وَأَعْلَمَكُمْ بِاللَّهِ أَنَا».
[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 20]
المزيــد ...
Imepokelewa kutoka kwa Aisha mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake amesema:
Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake anapowaamrisha anawaamrisha katika matendo yale wanayoyaweza, wakasema: Sisi hatuna nafasi kama yako ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu amekusamehe yaliyotangulia katika madhambi yako na yajayo, basi anachukia mpaka anaonekana usoni kuwa amechukia, kisha anasema: "Hakika mchamungu wenu na mwenye kumjua zaidi Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi ni mimi".
[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [صحيح البخاري - 20]
Anaeleza mama wa waumini Aisha radhi za Allah ziwe juu yake kuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake alikuwa anapowaamrisha watu amali miongoni mwa amali anawaamrisha kwa jambo ambalo ni jepesi kwao na si zito, kwa kuhofia wasijekushindwa kudumu nalo, na yeye pia anafanya mfano walile alilowaamrisha katika wepesi, lakini wao walimuomba kubebeshwa magumu, kwa kudhania kwao kuwa wana haja ya kuzidisha zaidi katika amali kwa sababu yeye amenyanyuliwa daraja zaidi. Wanasema: Hakika sisi hatuko katika hali kama ya kwako ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, kwani Mwenyezi Mungu amekusamehe yaliyotangulia katika madhambi yako na yajayo, basi anakasirika mpaka hasira inajulikana usoni kwake, kisha anasema: Hakika mchamungu wenu zaidi na mjuzi wenu kwa Mwenyezi Mungu ni mimi, basi fanyeni yale ninayowaamrisha.