+ -

عَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُما قَالَ:
كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِي سَفَرٍ، فَرَأَى زِحَامًا وَرَجُلًا قَدْ ظُلِّلَ عَلَيْهِ، فَقَالَ: «مَا هَذَا؟»، فَقَالُوا: صَائِمٌ، فَقَالَ: «لَيْسَ مِنَ البِرِّ الصَّوْمُ فِي السَّفَرِ»، وَفِي لَفْظٍ لِمُسلِمٍ: «عَلَيْكُمْ بِرُخْصَةِ اللهِ الَّذِي رَخَّصَ لَكُمْ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 1946]
المزيــد ...

Kutoka kwa Jaabir bin Abdillaah -radhi za Allah ziwe juu yao amesema:
Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika safari, akaona msongamano na mtu kazingirwa, akasema: "Nini hicho?", wakasema: Alikuwa kafunga swaumu, akasema: "Si katika wema kufunga safarini", na katika tamko la Muslim: "Chukuweni ruhusa ya Mwenyezi Mungu aliyokuruhusuni".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح البخاري - 1946]

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika safari, akaona mtu mmoja watu wamemkusanyikia na wamemzingira ili kumkinga na joto la jua na wingi wa kiu, akasema: Kapatwa na nini? Wakasema: Anaswaumu, akasema: Si katika wema kufunga safarini, Chukuweni ruhusa ya Mwenyezi Mungu aliyokuruhusuni.

Katika Faida za Hadithi

  1. Kumebainishwa wepesi wa Uislamu.
  2. Inafaa kufunga safarini, na pia inafaa kuchukua ruhusa ya kula.
  3. Inachukiza kufunga safarini ikiwa ataelemewa, madam hali haitomfikisha katika maangamivu.
  4. Amesema Nawawi: Si katika wema nyinyi kufunga mkiwa safarini: Maana yake: Ikiwa swaumu itawapa tabu juu yenu na mkahofia madhara, na mlolongo wa hadithi unaashiria maana hii.
  5. Kuwatilia umuhimu Mtume rehema na amani ziwe juu yake Maswahaba zake na kuuliza kwake hali zao.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Thai Kiassam الهولندية الغوجاراتية الدرية المجرية الجورجية المقدونية
Kuonyesha Tarjama
Ziada