+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«مَا مِنَ الأَنْبِيَاءِ نَبِيٌّ إِلَّا أُعْطِيَ مَا مِثْلهُ آمَنَ عَلَيْهِ البَشَرُ، وَإِنَّمَا كَانَ الَّذِي أُوتِيتُ وَحْيًا أَوْحَاهُ اللَّهُ إِلَيَّ، فَأَرْجُو أَنْ أَكُونَ أَكْثَرَهُمْ تَابِعًا يَوْمَ القِيَامَةِ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 4981]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake:
"Hakuna yeyote katika Manabii isipokuwa alipewa mfano wa yale waliyoyaamini watu, na hakika niliyopewa mimi ni wahyi (ufunuo) wa Mwenyezi Mungu alionifunulia, basi nataraji kuwa na wafuasi wengi kuliko wao siku ya Kiyama".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح البخاري - 4981]

Ufafanuzi

Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa Manabii wote Mwenyezi Mungu aliwapa nguvu na akawapa alama na miujiza iliyo nje na kawaida ya watu, watakayoitumia kama ushahidi juu ya unabii wao na kumpelekea kuamini atakayeishuhudia kwa kuwasadikisha, na kwamba yeye ameshindwa katika changamoto hiyo, kiasi kwamba hawezi kuizuia yeye mwenyewe binafsi, lakini anaweza kupinga akakaidi. Bali yeye rehema na amani ziwe juu yake alama yake na muujiza wake ni Qur'ani aliyomteremshia Mwenyezi Mungu kwa Wahyi; kwa namna ilivyokusanya miujiza ya wazi tena endelevu kwa wingi wa faida zake na kuenea kwa manufaa yake, kwa kukusanya kwake ujumbe na hoja na habari za yale yatakayotokea, manufaa yake yakamuenea aliyepo na asiyekuwepo na aliyepatikana na atakayepatikana, kisha akasema: Basi ninataraji kuwa na wafuasi wengi zaidi yao siku ya Kiyama.

Katika Faida za Hadithi

  1. Kumethibitishwa alama kwa Manabii, na hii ni katika huruma za Mwenyezi Mungu Mtukufu na fadhila zake juu Umma zote.
  2. Kumebainishwa ukubwa wa muujiza wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
  3. Kumebainishwa ukubwa wa nafasi ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake na ubora wake juu ya Manabii wengine.
  4. Amesema bin Hajari katika kauli yake: "Bali imekuwa kile nilichopewa kuwa ni wahyi alioniteremshia Mwenyezi Mungu kwangu mimi": Na makusudio yake si kubana miujiza yake hapa, wala kuwa hakupewa miujiza waliopewa waliomtangulia, bali makusudio yake ni kuwa ndio muujiza mkubwa ambao ulikuwa maalumu kwake peke yake pasina mwingine.
  5. Amesema Nawawi: "(Nataraji mimi kuwa na wafuasi wengi zaidi yao" Hii ni alama miongoni mwa alama za Unabii, kwani alilieleza hili rehema na amani ziwe juu yake katika zama za Waislamu wachache, kisha Mwenyezi Mungu Mtukufu akaleta neema na akawafungulia Waislamu na akawabariki mpaka Uislamu ukafika mbali na ukapanuka kwa Waislamu kwa kiwango hiki kinachofahamika, tunamshukuru Mwenyezi Mungu.
Tafsiri: Lugha ya Kiindonesia Kibangali Kivetenamu Kikurdi Kihausa Kireno Thai Kiassam الهولندية الدرية المجرية الجورجية المقدونية
Kuonyesha Tarjama