عن عبد الله ابن عباس رضي الله عنهما أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «إن الله تَجَاوزَ لِي عن أمتي الخطأَ والنِّسْيانَ وما اسْتُكْرِهُوا عليه».
[ضعيف] - [رواه ابن ماجه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillah bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika Mwenyezi Mungu ameniondolea mimi kwa umma wangu (madhambi ya) kukosea na kusahau, na yale waliyolazimishwa".
Miongoni mwa huruma ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa umma huu ni kuusamehe madhambi ya kukosea -Nayo ni yale ambayo hawajakusudia miongoni mwa maasi- na kusahau wajibu wao au kufanya maharamisho, lakini baadaye akikumbuka wajibu wake anaufanya, hivyo hivyo hata yale waliyolazimishwa na wakatezwa nguvu kuyafanya katika maasi na makosa ya jinai, Akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na hakukufanyieni juu yenu uzito katika dini".